Mawingu ya Magellan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mawingu ya Magellan

Mawingu ya Magellan (ing. Magellanic Clouds) ni galaksi mbili ndogo zinazoonekana kama doa angavu angani kwa macho matupu ya watazamaji kwenye angakusi ya Dunia. Hazionekani kwenye nusutufe ya kaskazini ya Dunia.

Mawingu ya Magellan ni sehemu ya kundi janibu la galaksi yakizunguka Njia Nyeupe. Hayana umbo maalum. Yanaitwa

Mawingu hayo yalijulikana tangu kale kati ya mataifa ya nusutufe ya kusini na kupokea majina. Ushuhuda wa kwanza wa kimaandishi upo katika kitabu cha mwanaastronomia Al Sufi juu ya nyota kilichotungwa mnamo mwaka 964 BK. Mzungu wa kwanza aliyeyaeleza alikuwa Ferdinand Magellan alipozunguka Dunia kwenye mwaka 1519.

Katika darubini, mawingu hayo yanaonekana kama galaksi yenye nyota, nebula na mafungunyota ndani yake.