Nenda kwa yaliyomo

Martin de Porres

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Martin wa Porres)
Picha hii ya Martin des Porres iko katika monasteri ya Mt. Ann mjini Lima.
Sura yake halisi.

Martin de Porres, O.P. (15793 Novemba 1639) alikuwa bradha wa Shirika la Wahubiri katika nchi ya Peru.

Akiwa mtoto chotara wa kabaila Mhispania Juan de Porres na binti mwenye asili ya Afrika Anna Velasquez hakutambuliwa na baba yake akalelewa na mama kwa shida, lakini alipata kuwa msaidizi wa daktari akijifunza hivyo elimu ya matibabu [1].

Mwaka 1594 alijiunga na watawa Wadominiko akaendelea kuhudumia kwa ukarimu wagonjwa wa matabaka na rangi zote, lakini hasa fukara.

Alikuwa na kipaji cha uponyaji ambacho kiliwasaida watu wengi. Kutokana na upendo aliowaonyesha watu wote aliheshimiwa sana na taarifa za uponyaji wa ajabu zilianza kuenea.

Akiwa na juhudi katika kufunga chakula, kufanya toba na kusali, aliishi kwa usahili na unyenyekevu.

Mwaka 1837 alitangazwa mwenye heri na Papa Gregori XVI, halafu tarehe 6 Mei 1962 akatangazwa na Papa Yohane XXIII kuwa mtakatifu[2].

Sikukuu yake ni tarehe 3 Novemba kila mwaka[3].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/29900
  2. Sehemu ya hotuba yake siku hiyo imetafsiriwa kwa Kiswahili katika Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 405-407.
  3. Martyrologium Romanum
  • BENEDICTINE FATHERS – Rafiki Martin, Habari za Maisha ya Mtakatifu Martin De Porres O.P. – Kipigo Chapa cha Tano ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1990 – ISBN 9976-63-057-3
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 387-388
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 342-343

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.