Nenda kwa yaliyomo

Martin Lynn

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Martin Lynn (31 Agosti 195115 Aprili 2005) alikuwa mwanahistoria na msomi wa Uingereza na Nigeria, aliyebobea katika Historia ya Afrika. Baada ya kufundisha katika Chuo Kikuu cha Ilorin,Lynn alihamia Chuo Kikuu cha Queen's Belfast mwaka 1980. Hapo, Lynn alifundisha historia ya Uingereza na Milki yake, na baadaye historia ya Afrika na China. Utaalamu wake mahususi wa kitaaluma ulikuwa katika historia ya kiuchumi ya Afrika Magharibi.[1] Mwaka 2002,Lynn aliteuliwa kuwa Profesa wa Historia ya Afrika akiwa mtu wa kwanza kushika nafasi ya uprofesa wa historia ya Afrika nchini Ireland. [2]

  1. admin (2018-06-17). "Prof. Martin Lynn". Africa and Africans @ QUB (kwa Kiingereza (Uingereza)). Iliwekwa mnamo 2025-10-15.
  2. "Professor Martin Lynn August 31, 1951-April 15, 2005". The Times (kwa Kiingereza). 18 Mei 2005. Iliwekwa mnamo 30 Oktoba 2021.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Martin Lynn kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.