Nenda kwa yaliyomo

Marie-Claire Faray

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Marie-Claire Faray ni mwanaharakati na mtetezi wa haki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo . Anaishi London ambako anajihusisha na harakati za kukomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake. [1] .

Anasema kwamba, ingawa wanawake wa Kongo walitumiwa kama uwanja wa vita wakati wa vita nchini DRC, leo hii wameenguliwa kutoka katika mchakato wa amani.[2] .

Utoto wa mapema na elimu

[hariri | hariri chanzo]

Faray alipata shahada yake ya kwanza ya sayansi katika Chuo Kikuu cha Metropolitan cha London na shahada ya uzamili ya sayansi katika Shule ya Afya na Tiba ya Kitropiki ya London. Pia alisoma katika Chuo Kikuu cha Queen Mary, pia jijini London. London [3] .

Faray anafanya kazi kama mshauri wa masuala ya taarifa za kitabibu kwa ngazi ya uzamili na mtafiti wa kisayansi wa magonjwa ya kuambukiza katika Chuo Kikuu cha Queen Mary cha London na Hospitali ya Barts.[4] . Faray anatetea kuundwa kwa miongozo ya kimataifa inayoheshimu sheria na serikali [5] akiendesha kampeni dhidi ya ukatili kwa wanawake barani Afrika na kwa ajili ya amani na haki za binadamu kwa ujumla. [6] .

Faray anashiriki katika kuendeleza Mkataba wa Maputo kwa ajili ya haki za wanawake wa Afrika. Mojawapo ya malengo yake makuu ni kuhakikisha haki za msingi za wanawake wote na usalama wao, kwa mujibu wa vifungu vya 3, 17, 18, 19 na 20 vya Azimio la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu, kote barani Afrika ifikapo mwaka 2020, kama sehemu ya harakati za Muongo wa Wanawake wa Afrika.[5] . Yeye ni makamu wa rais wa tawi la Uingereza la Shirika la Kimataifa la Wanawake kwa Ajili ya Amani na Uhuru[6] na yuko katika kamati ya utendaji ya Common Cause UK, jukwaa ambalo linakuza wanawake wa Kongo nchini Uingereza [4] . Yeye pia ni mwanachama wa muungano wa Million Women Rise, muungano wa kitaifa wa wanawake . Mnamo Desemba 16, 2007, Faray alianzisha tawi la WILPF huko Kinshasa . Yeye ni miongoni mwa wanawake wa Kongo walioko mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko nchini Kongo[7] .

Umoja wa Mataifa

[hariri | hariri chanzo]

Faray alishiriki katika mkutano wa kila baada ya miaka miwili wa Mataifa ya Umoja wa Mataifa mwaka 2008 kujadili uhusiano kati ya silaha ndogo ndogo na unyanyasaji dhidi ya wanawake barani Afrika [8] .

Faray anaishi jijini London pamoja na binti zake wawili. [5] .

  1. "Establishing equal rights across Africa" (kwa Kiingereza). 26-11-2012. Iliwekwa mnamo 2023-11-11. {{cite web}}: Check date values in: |date= (help).
  2. "Congo women - violence in war and in peace | Pambazuka News" (kwa Kiingereza). 2016-03-04. Iliwekwa mnamo 2023-11-11.
  3. "GUEST SPEAKERS". metimun2011.weebly.com. Iliwekwa mnamo 20 Novemba 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. 1 2 "Jan 30 – Marie Claire Faray – Congolese Women's Resistance, Past and Present". Congolive.org. 30 Januari 2016. Iliwekwa mnamo 25 Machi 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. 1 2 3 "Our March Interview with Marie Claire Faray-Kele". Makeeverywomancount.org. 1 Machi 2011. Iliwekwa mnamo 25 Machi 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  6. 1 2 "'Give African women a voice,' say activists". CNN. 30 Novemba 2012. Iliwekwa mnamo 25 Machi 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  7. Marie Claire Faray: The History of Congolese Women's Resistance from Past to Present (kwa Kifaransa). Iliwekwa mnamo 2023-11-11.
  8. "TALKS CONCLUDE ON MARKING, TRACING ILLEGAL SMALL ARMS, LIGHT WEAPONS, AS BIENNIAL MEETING OF STATES SEEKS TO STRENGTHEN POLITICALLY-BINDING GLOBAL INSTRUMENT". un.org. Iliwekwa mnamo 20 Novemba 2016.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)