Maria Wilman
Maria Wilman (29 Aprili 1867 - 9 Novemba 1957) alikuwa mwanajiolojia na mtaalamu wa mimea kutoka Afrika Kusini. Ni Mkurugenzi wa kwanza wa Makumbusho ya McGregor huko Kimberley, nchini Afrika Kusini, na mwanamke wa pili kutoka Afrika Kusini kusomea katika Chuo Kikuu cha Cambridge nchini Uingereza.
Wilman alizaliwa Beaufort West tarehe 29 Aprili mwaka wa 1867, akiwa mtoto wa tano kuzaliwa kati ya watoto wa kike tisa wa Herbert Wilman na Engela Johanna Neethling. Baba yake alikuwa mhamiaji kutoka Yorkshire, nchini Uingereza, aliyekuja nchini Afrika Kusini, na alifanya kazi kama Mbunge wa Beaufort West katika Bunge la Cape chini ya Waziri Mkuu John Molteno.
Maisha ya mwanzo
[hariri | hariri chanzo]Wilman alizaliwa Beaufort West tarehe 29 Aprili mwaka wa 1867, alikwa mtoto wa tano kuzaliwa kati ya watoto wa kike tisa wa Herbert Wilman na Engela Johanna Neethling. Baba yake alikuwa mhamiaji kutoka Yorkshire nchini Uingereza, na alifanya kazi kama Mbunge wa Beaufort West katika Bunge la Cape chini ya Waziri Mkuu John Molteno.
Elimu
[hariri | hariri chanzo]Wilman kwanza alihitimu katika Shule ya Good Hope Seminary jijini Cape Town. Mnamo mwaka 1885, alijiunga na Chuo Kikuu cha Cambridge na alikuwa mwanamke wa pili kutoka Afrika Kusini kujiunga katika chuo hicho. Alimaliza mtihani wa sayansi asilia katika masomo ya jiolojia, madini, na kemia katika Chuo cha Newnham, Cambridge mnamo mwaka 1888, na MA katika botania mnamo mwaka 1895. Hata hivyo, wanawake hawakupewa shahada rasmi hadi miaka ya 1930, kwa hivyo Wilman hakupokea MA yake kutoka Cambridge hadi Novemba mwaka wa 1931
Mwaka wa 1939, alipewa udaktari wa heshima katika sheria kutoka Chuo Kikuu cha Witwatersrand jijini Johannesburg.
Mkurugenzi wa Jumba la Makumbusho la McGregor huko Kimberley
[hariri | hariri chanzo]Aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa kwanza wa Jumba la Makumbusho la McGregor lililoanzishwa hivi karibuni huko Kimberley mnamo mwaka wa 1908. Pia alianzisha bustani ya mimea huko mwaka huo huo na kuanza kulima mkusanyiko wake wa mimea ya kikanda, ambayo inahusisha sampuli muhimu kutoka Rasi ya Kaskazini. Aliimarisha uhusiano na wakusanyaji wa sampuli za wenyeji, kama vile Constance Georgina Adams, ambaye alianzisha urafiki naye wa muda mrefu. [1]
Kazi aliyokuwa akifanya ya mimea huko McGregor ilisababisha kuchapishwa kwa Orodha ya Awali ya Mimea na Mimea ya Maua ya Griqualand West (mwaka wa 1946). Pia alianzisha miti ya mesquite na kurrajong huko Kimberley na kushiriki mbegu za nyasi za nchini Afrika Kusini na taasisi na mashirika nchini Marekani. Baadhi wamehusisha aina hizi za majani na kufufua baadhi ya maeneo ya Dust Bowl nchini, hasa katika jimbo la Texas .
Wilman aliamua kuacha kazi kutoka kuwa ukurugenzi wa McGregor mnamo mwaka wa 1947, lakini aliendelea kufanya kazi katika masomo yake ya jiolojia na mimea huko. Alistaafu kabisa kutoka kwenye jumba la makumbusho mnamo mwaka wa 1953 na akaenda kuishi George. Wilman alifariki hapo mnamo 9 Novemba mwaka wa 1957. Hakuwahi kuoa.
Urithi
[hariri | hariri chanzo]Mimea chache zimepewa majina kwa heshima yake, ikiwa ni pamoja na Wilman lovegrass ( Eragrostis superb ), <i id="mwkg">Watsonia wilmaniae</i>, Stapelia wilmaniae, Ruschia wilmaniae, Hereroa wilmaniae, na Nananthus wilmaniae .
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Rall, Maureen (2002). Petticoat Pioneers: The History of the Pioneer Women who Lived on the Diamond Fields in the Early Years. Kimberley: Kimberley Africana Library. uk. 117. ISBN 978-0-62027-613-9.