Mamalia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mammalia)
Mammalia
Kangaruu ni mamalia wa Australia
Kangaruu ni mamalia wa Australia
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Faila: Chordata
Ngeli: Mammalia
Ngazi za chini

Mamalia ni wanyama ambao wanawanyonyesha watoto wao maziwa kwa kutumia viwele vyao.

Wana damu moto na kupumua kwa mapafu.

Kuna takriban spishi 5,400 za mamalia. Spishi 5 kati ya hizo wanataga mayai, lakini wengine wote wanazaa watoto hai.

Ukubwa unatofautiana sana, kuanzia spishi ndogo aina ya popo mwenye urefu wa sentimita 4 pekee hadi spishi kubwa nyangumi buluu mwenye urefu wa mita 33.

Uainishaji[hariri | hariri chanzo]

Mamalia ni ngeli ya faila Kodata.

Ngeli yao hugawiwa katika nusungeli mbili:

  • Prototheria ni mamalia wanaotaga mayai au kubeba watoto wao ndani ya mfuko wa mwilini kwa muda fulani baada ya kuzaa
  • Theria ni mamalia wa kawaida na spishi nyingi zimo humo.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mamalia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.