Majeshi ya Ulinzi ya Kenya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Brigedia Jenerali Leonard Ngondi wa Jeshi la Kenya (kushoto) akisalimia Luteni Kanali Steve Nichols wa Marekani (kushoto) wakiwa Camp Lonestar, Kenya, mwaka 2006.

Majeshi ya Ulinzi ya Kenya (kwa Kiingereza: Kenya Defence Forces, kifupi: KDF) ni vikosi vya kijeshi vya Jamhuri ya Kenya: Jeshi la Ardhi la Kenya, Jeshi la Wanamaji la Kenya, na Jeshi la Anga la Kenya huunda vikosi vya ulinzi.

Muundo wa sasa wa majeshi hayo ulifanywa mwaka 2010 na Katiba ya Kenya ya 2010. Aidha, KDF huongozwa na Sheria ya Majeshi ya ulinzi ya Kenya ya mwaka 2012 .[1]

Rais wa Kenya ndiye Amirijeshi mkuu.

Mara kwa mara, vikosi hivyo vimehusika katika ulinzi wa amani duniani. Tume ya Waki, ilipongeza utayari wake na kuvichukulia "kuwa walitimiza wajibu wake vizuri." katika vurugu ya mwaka 2008[2] Hata hivyo, kumekuwa na madai makubwa ya ukiukwaji wa haki za binadamu, kama vile, wakati wa shughuli za kukabiliana na waasi katika eneo la Mlima Elgon[3] na pia katika wilaya ya Mandera ya kati.[4]

Historia[hariri | hariri chanzo]

1896 hadi 1900[hariri | hariri chanzo]

Kati ya mwaka 1896 hadi 1900, East African Rifles walitumika kutimiza sera za kikoloni za Uingereza. Kwa ushirikiano na Meja Cunningham wa Uganda Rifles, vita vilipangwa dhidi ya Wanandi ambao walikuwa wamepinga vikali ukoloni. 

East African Rifles pia ilitumia askari Uganda Rifles kusaidia kukandamiza uasi wa vikosi vya Sudani katika Uganda

Mwaka 1901, serikali ya Uingereza iliamua kupanga vikosi vyote katika Afrika ya Kati, Afrika ya Mashariki, Uganda na Somalia ya Kiingereza chini ya amri moja. Luteni Kanali Manning, afisa katika India Corps aliteuliwa Mkaguzi Mkuu wa vikosi vyote na kupandishwa katika ngazi ya jenerali.

Baada ya kuunganishwa kwa majeshi yote katika milki za Afrika ya Kati na ya Mashariki za Uingereza, rejimenti iliundwa tarehe 1 Januari 1902 na kuitwa "King's African Rifles". Muundo wa hilo jeshi ulikuwa kama ifuatavyo:

  • Makampuni 8 ya 1 Central African Rifles yakawa Kikosi 1 cha King's African Rifles.
  • Makampuni 6 ya 2 Central African Rifles yakawa Kikosi 2 cha King's African Rifles.
  • Makampuni 7 na kampuni moja ya ngamia ya East African Rifles yakawa Kikosi 3 cha King's African Rifles.
  • Makampuni 9 ya Uganda Rifles yakawa Kikosi 4 cha King's African Rifles.
  • Makampuni 4 ya Sanjari ya Uganda Rifles yakawa Kikosi 5 Kings African Rifles.

1902 hadi 1963[hariri | hariri chanzo]

Tarehe 1 Aprili 1902, 3 KAR ilihamisha makao makuu kutoka Mombasa hadi Nairobi, na pamoja na 4 KAR na 5 KAR, vilikuwa vikitumiwa na serikali ya kikoloni ya Uingereza katika vita dhidi ya waliokuwa wakipinga utawala wa Uingereza.

Mwaka 1904 5 KAR kilivunjwa kwa sababu ya gharama za utunzaji na pia kwa sababu Waingereza walihisi kuwa upinzani dhidi ya utawala wao ulikuwa umedhibitiwa. Kilirejeshwa tena mwaka 1916 na kuwekwa Meru.

Mwaka 1926, 5 KAR ilivunjwa tena na rangi zao zikakabidhiwa 3 KAR zilindwe. Tarehe 1 Machi 1930 kitengo kilirejeshwa tena upya, na kurudishiwa rangi zake Nairobi. Baada ya Vita vya pili vya Dunia vikosi vyote vilitumiwa na serikali ya kikoloni dhidi ya uasi wa Mau Mau.

Katika alfajiri ya uhuru wa Kenya, Bunge la Taifa lilipitisha muswada (Miswada ya Kenya, 1963) kufanya marekebisho ya hadhi ya majeshi Kenya.

Vitengo vilivyokuwa vya King's African Rifles vilifanywa kuwa Vikosi vya Jeshi la Kenya na serikali huru ya Kenya ikapewa uwezo wa kuteua majina ya vitengo itakavyo kuanza thenashara alfajiri 12 Disemba 1963. Hivyo 3 KAR, 5 KAR, na 11 KAR vikawa 3 Kenya Rifles, 5 Kenya Rifles, na 11 Kenya Rifles mtawalia. Mabadiliko ya King's African Rifles Kenya Vikosi vya Kijeshi juu ya usiku wa manane wa tarehe hiyo ilikuwa hatua kubwa katika msingi wa leo wa vitengo vya Jeshi la Kenya.

1963 hadi leo[hariri | hariri chanzo]

Kati ya mwaka 1963 na mwaka wa 1967, Kenya ilipigana katika Vita vya Shifta vilivyokuwa dhidi ya Wakenya Wasomali waliotaka kuungana na jamaa zao katika Jamhuri ya Somalia.[5]

Jioni ya tarehe 24 Januari 1964, kukosa kujitokeza kwa Waziri Mkuu wa Kenya na kuonekana kwenye televisheni, ambapo wadogo wa wanajeshi wa 11 Kenya Rifles walikuwa wakitarajia hotuba ya televisheni wakiwa na matumaini ya tangazo la kuongezewa mshahara, kulisababisha wanajeshi hao kuasi.[6] Serikali ilifanya vikao viwili vya mahakama ya kijeshi kuwahukumu wanajeshi 43.

Baada ya uasi na kufuatia vikao vya mahakama ya kijeshi, 11 Kenya Rifles kilivunjwa.[7] Kikosi kipya, 1 Kenya Rifles, kiliundwa kutumia wanajeshi 340 kutoka Lanet waliokuwa wamekubaliwa na Idara ya Uchunguzi wa Jinai (CID) kuwa hawakushiriki katika uasi. 

Vikosi vya Uingereza vilitoka nchini tarehe 12 Disemba 1964 baada ya makubaliano yaliyofanywa tarehe 3 Juni 1964 kati ya Kenya na Katibu wa Dola kwa Uhusiano wa Jumuia ya Madola. Uingereza ilikuwa isaidie jeshi, iifadhili na itoe mafunzo kwa kikosi kipya cha Jeshi la Anga la Kenya na itengeneze Jeshi la Wanamaji la Kenya. Pia, ilikuwa itoe vitengo vya Jeshi la Kifalme la Hewani na vya Jeshi la Ardhi kuongeza usalama katika eneo la Mashariki Kaskazini. Mikopo muhimu ilikuwa ifutwe, na mali nyingi ikabidhiwe kwa Serikali ya Kenya. Kwa upande wao, ndege kutoka Uingereza zingeweza kupitia Kenya, meli za vikundi vya manowari vya Mashariki ya Mbali na vitengo vingine vya Jeshi la Kifalme la Wanamaji vingeweza kutembelea Mombasa, vifaa vya mawasiliano vingeweza kutumika hadi mwaka 1966, na vikosi vingeweza kufanya mazoezi nchini Kenya mara mbili kwa mwaka.[8] Vikosi vya mafunzo viliendelea kutumwa nchini hadi mwaka 2015, vikisimamiwa na Kitengo cha Jeshi la Mafunzo cha Uingereza Kenya.

Timothy Parsons aliandika katika 2003:[9]

'...Kenyatta hakuwa na wasiwasi kuhusu hali ya uaminifu wa kisiasa wa Jeshi la Kenya kwa sababu washauri wataalamu waandamizi Waingereza wa kijeshi waliitendesha kama KAR miaka ya 1960. Kufuatia masomo ya wanajeshi kutoka Lanet, maafisa wa Kiafrika walichukua amri ya uendeshaji wa vitengo vyote vikuu, lakini timu ya mafunzo ya Uingereza bado ilikuwa ikisimamia Jeshi la Kenya kwa muda mrefu wa mwongo huo. Pia, kwa kiasi kikubwa, utaratibu wa ulinzi usio rasmi uliofanywa pamoja na Uingereza ulihakikisha kwamba Kenyatta angeweza kutegemea msaada wa moja kwa moja kutoka Jeshi la Uingereza kungetokea uasi wa jeshi au jaribio la thaura.' (Imetafsiriwa)

Miezi kadhaa baada ya Brigedia Mwingereza A. J. Hardy kumkabidhi amri ya Jeshi la Kenya Brigedia Joseph Ndolo tarehe 1 Desemba 1966, ushawishi wa Uingereza ulidhihirika wakati Meja Jenerali Bernard Penfold aliteuliwa kama Mkuu wa Majenerali, nafasi mpya kama afisa mwandamizi vikosi vyote vya jeshi.[10] Ndolo alichukua nafasi ya Penfold kama Mkuu wa Majenerali mwaka 1969, akastaafu tarehe 24 Juni 1971 baada ya kukisiwa alihusika katika njama za thaura iliyodaiwa kupangwa na Joseph Owino. Baada ya hayo, wakuu wa jeshi walikuwa wakipiga taarifa moja kwa moja kwa Waziri wa Ulinzi, James Gichuru.[11]

Nafasi ya Mkuu wa Majenerali ilijazwa tena miaka saba baadaye wakati Daniel arap Moi alimpandisha hadhi Luteni Jenerali Jackson Mulinge kutoka Kamanda wa Jeshi hadi Mkuu wa Majenerali mwezi Novemba 1978.[12] Mahamoud Mohamed alichukua nafasi ya Mulinge katika mwaka wa 1986, na alikuwa Mkuu wa Majenerali hadi 1996. Nafasi ya Mohamed ilichukuliwa na Jenerali Daudi Tonje, Mkuu wa Majenerali mwaka 1996-2000. (Hornsby 554)

Kutoka miaka ya 1990, Jeshi la Kenya lilijihusisha na operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.[13] Misheni ya kwanza ya ulinzi amani ya Kenya ilikuwa Namibia na UNTAG mwaka 1989 hadi 2001. Vikosi vya Kenya vilihusika katika misheni za UNTAG, UNOSOM, UNPROFOR, UNCRO (Kroasia), UNTAES, UNOMIL, UNPREDEP katika Jamhuri ya Masedonia(1996-1999), MONUA huko Angola (1997-1999) na UNTAET huko Timor ya Mashariki (1999-2001).[14] Mwaka 2000, wanawake walijumuishwa ndani ya vitengo vya kawaida vya jeshi na Kitengo cha Huduma ya Wanawake kuvunjwa.

Katika karne ya 21, Wizara ya Ulinzi ni sehemu ya zana za Urais. Rais huteua na hustaafisha maafisa waandamizi kutumia mamlaka yake kama Amirijeshi Mkuu. Waziri wa Ulinzi husimamia Baraza la Kitaifa la Ulinzi. Mkuu wa Majenerali ni kiongozi mtawala, mtendaji na mtoa mbinu. Kulingana na Katiba ya mwaka 2010, majeshi ya ulinzi hayawezi kutumiwa ndani mwa Kenya bila idhini ya Bunge.

Baada ya matayarisho kati ya maafisa wa kijeshi wa Kenya na Somalia mjini Dhobley mwaka 2011,[15] vitengo vya Jeshi la Kenya vilivuka mpaka kuanzisha Operesheni Linda Nchi dhidi ya Al-Shabaab Kusini mwa Somalia.[16] Misheni iliongozwa na majeshi ya Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia. Mwezi Juni 2012, Majeshi ya Kenya yalijumuishwa ndani ya AMISOM.[17]

Jeshi la Kenya[hariri | hariri chanzo]

Helikopta aina ya MD 500 Defender juu ya Duka kuu la Westgate wakati wa shambulio la mwaka 2013.

Wizara ya Ulinzi huorodhesha vitengo na huduma zifuatazo:[18]

Miundo ya Jeshi la Kenya[hariri | hariri chanzo]

  • Wanajeshi wa Miguu wa Jeshi la Kenya
  • Wanajeshi wa Kuruka wa Jeshi la Kenya
  • Hifadhi ya Ala za Jeshi la Kenya (hujumuisha Batalioni 78 ya Vifaru, Isiolo)
  • Vifyatuzi vya Jeshi la Kenya (hujumuisha Batalioni 78 ya Vifyatuzi)
  • Wahandisi wa Jeshi la Kenya
  • Batalioni ya Farasi na Hewani ya 50

Huduma za Jeshi la Kenya[hariri | hariri chanzo]

  • Wanajeshi Wahamishaji vifaa wa Jeshi la Kenya
  • Wanajeshi Wasafirishaji wa Jeshi la Kenya
  • Uhandisi Mitambo na Umeme
  • Kenya Corps Jeshi ya Ishara
  • Jeshi La Polisi 
  • Jeshi la Elimu
  • Batalioni ya Matibaby
  • Makonstebo wa Jeshi

Jeshi la Wanahewa na Nevi[hariri | hariri chanzo]

Jeshi la Wanahewa la Kenya liliundwa mwaka 1966 na likaasi mwaka 1982.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

  1. Ministry of Defence. "Kenya Defence Forces Act - No. 25 of 2012". National Council for Law Reporting. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2018-10-03. Iliwekwa mnamo 6 May 2014.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. "Microsoft Word - ~8860467.doc" (PDF). Web.archive.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 20 December 2008. Iliwekwa mnamo 2017-07-10.  Unknown parameter |df= ignored (help); Check date values in: |archivedate= (help)
  3. "MT. ELGON: POLICE ACTION IS AN AFFRONT TO THE, POWERS AND MANDATE OF KNCHR, A VIOLATION OF THE LAW AND AN ATTEMPT TO COVER UP THE TORTURE IN MT. ELGON" (PDF). Web.archive.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 14 February 2012. Iliwekwa mnamo 2017-07-10.  Unknown parameter |df= ignored (help); Check date values in: |archivedate= (help)
  4. "Security men accused of torture and rape - Daily Nation". Nation.co.ke. 2008-11-01. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2017-07-03. Iliwekwa mnamo 2017-07-10. 
  5. Bruce Baker, Escape from Domination in Africa: Political Disengagement & Its Consequences, (Africa World Press: 2003), p.83
  6. Timothy Parsons, The 1964 Army Mutinies and the Making of Modern East Africa, 120.
  7. Parsons, The 1964 Army Mutinies, 161.
  8. Hornsby, 98-99.
  9. Timothy Parsons, 'The 1964 Army Mutinies and the Making of Modern East Africa,' Greenwood Publishing Group, 2003, ISBN 0325070687, 169.
  10. Hornsby, Charles (2012). Kenya: A History Since Independence. London/New York: I. B. Tauris. uk. 180. ISBN 978-1-84885-886-2. 
  11. Hornsby, 228-229.
  12. Hornsby, 335-6.
  13. Hornsby, 554.
  14. Dr. Vince Sinning. "PEACEKEEPING OPERATIONS: Kenya Mission to the United Nations in New York, USA". Web.archive.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 27 September 2013. Iliwekwa mnamo 2017-07-10.  Unknown parameter |df= ignored (help); Check date values in: |archivedate= (help)
  15. "Kenya launches offensive in Somalia", 16 October 2011. Retrieved on 2 May 2015. 
  16. "Joint Communique – Operation Linda Nchi". Kenya High Commission, Tanzania. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 14 October 2013. Iliwekwa mnamo 25 September 2013.  Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  17. "Kenya: Defense Minister appointed as acting Internal Security Minister", 19 June 2012. Retrieved on 20 June 2012. Archived from the original on 30 November 2012. 
  18. "The Kenya Army Formations". Kenya Government, Ministry of State for Defence. Iliwekwa mnamo 9 August 2011.  Check date values in: |accessdate= (help)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]