Majadiliano:Windhoek

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Oliver, nimebadilisha picha kidogo (usipopenda basi rudisha hali ya awali) ili nikuonyeshe mambo machache ilhali wewe ni mgeni:

a) ukinakili picha na ukitaka maandishi yaonekane pamoja na picha: basi hakikisha ya kwamba |thumb| iko mara baada ya jina la picha yenyewe >> Image:Windhoek-Skyline.jpg|thumb|. Amri hii inasababisha mraba uonekane pamoja na nafasi ya maandishi.Maelezo ni mwisho kabisa. Nimeweka sasa "|Kitovu cha mji wa Windhoek"

b) angalia unataka mwelekeo gani: left - center - right

c) kuweka viungo : ukifungua makala tuseme ya Kiingereza - boyeza edit (kama ukitaka kuazima picha na kunakili mstari wake) - nenda mwishoni kabisa - utaona orodha ya viungo: af:Windhoek ar:ويندهوك da:Windhoekde:Windhuk na kadhalika.

sasa unanakili viungo vya lugha nyingine na kupachika katika makala yako mwisho kabisa.

Unaweza kuongeza shughuli mbili: a) mara umeshafungua Kiingereza/edit basi weka mstari mpya baada ya "k" na ingiza kiungo chako kipya yaani "sw:Windhoek" halafu weka [[ ]]

b) katika makala yako Kiingereza haimo (kwa sababu umenakili pale) kwa hiyo unafanya mstari mpya kwenye "e" na kuingiza "en:Windhoek" halafu [[ ]]

Naona si vigumu hata usipojisikia mtaalamu wa mitambo nimeshaone unajifunza haraka sana - kwa maswali mengine mimi humwuliza Matt Crypto au Marcos. --Kipala 13:44, 2 May 2006 (UTC)