Wanyiha

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wanyiha ni kabila la watu wa Tanzania (Wilaya ya Mbozi, mkoa wa Songwe). Katika wilaya ya Mbozi Wanyiha wengi hupatikana magharibi, hasa vijiji vya Itaka, Nambizo, Mbozi mission, Shiwinga, Igamba na maeneo mengine ya huko. Pia upande wa mashariki utawakuta katika vijiji vya Nyimbili, Idiwili Hezya n.k.

Tena wako Zambia, Malawi na sehemu nyingine. Kwa jumla ni zaidi ya 600,000.

Inasadikiwa Wanyiha ni moja ya makabila ya Kibantu yenye asili ya Afrika Kusini (Wazulu au Wangoni).

Lugha yao ni Kinyiha. Kabila hili katika utamkaji wa maneno hufanana sana na Wasafwa, Wamalila, pia Wanyamwanga.

Wanyiha ni wapole na wasikivu. Baadhi ya koo za Kinyiha ni Mwashiozya, Mwashiuyà, Mwembe, Nzunda, n.k. Chifu wa Wanyiha ni Mwene.

Wanyiha wamezungukwa na makabila mbalimbali wakiwemo Wasafwa, Wandali, Wanyakyusa, Wabungu na Wanyamwanga.

Wanyiha walio wengi ni wakulima: zao kuu la chakula ni mahindi wakati zao kubwa la biashara ni kahawa.

wanyiha wanaposalimiana husema: Mwakataa... Halafu mtu wa pili hujibu: Ena..kabila hili wao huamini mgeni wa jirani ni mgeni wa wote .

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Arnold, Bernd; Steuer und Lohnarbeit im Südwesten von Deutsch Ostafrika
  • Bauer, Andreus; Emperial Rugaruga ("Raise the Flag of War")
  • Becker, Perbandt, Richelmann & Schmidt, Steuber. Hermann von Wissmann, Deutschlands Grösster Africaner
  • Brock, Beverly; The Nyiha of Mbozi
  • Willis, Roy G.; The Fipa and Related Peoples
  • Weule, Karl; Deutsches Kolonial Lexicon, Band IIIs. 673
Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wanyiha kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.