Utani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Utani ni maneno ya mzaha yenye ukweli ndani yake. Utani kama kipengele kimojawapo cha sanaa na maigizo huonesha uhusiano mwema wa jamii unaowawezesha wanajamii hao kufanyiana maneno ya mzaha na hata kuchukuliana vitu bila kukasirikiana.

Utani unaweza kuwa kati ya mtu na mtu, ukoo na ukoo au kabila na kabila. Katika nchi ya Tanzania umechangia sana kumaliza au kuepusha vita na shari nyingi baada ya makabila adui kuamua kutambuana kama watani, k.mf. Wangoni na Wahehe.

Umuhimu wa utani
Hasara za utani
  • Husababisha ugomvi katika jamii
  • Huleta hasara kwa kuchukuliana vitu bila malipo
  • Husababisha kuvunjiana heshima miongoni mwa wahusika

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

  • Ufafanuzi wa kamusi kuhusu utani katika Wikamusi
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Utani kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.