Tokyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mji wa Tokyo








Jiji la Tokyo
Faili:Flag of .png
Bendera
Nchi Japani
Kanda Kantō
Mkoa Tokyo
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 12,976,698
Tovuti:  www.tokyo.jp
Bendera ya Tokyo
Bendera ya Tokyo
Mahali pa Tokyo katika Japani
Shibuya
Marunouchi
Idadi ya wakazi

Jiji la Tokyo (東京都) ni mji mkuu wa Japani. Takriban watu milioni 12 huishi katika jiji hilo ambao ni sawa 10% ya Wajapani wote. Rundiko la mji lina wakazi milioni 35 na ni rundiko kubwa duniani.

Tokyo ni kitovu cha Japani upande wa biashara, uchumi na siasa.

Mahali pa jiji ni tambarare ya Kanto kando ya hori ya Tokyo.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Awali Tokyo iliitwa "Edo". Wakati ule Kyoto ilikuwa mji mkuu rasmi na mahali pa Tenno au Kaisari wa Japani. Edo ilikuwa mwanzoni bandari ndogo tu. Ilianza kukua baada ya kuwa makao makuu ya Mashogun waliokuwa viongozi wa kijeshi katika Japani.

Katika karne ya 19 Tenno Meiji alihamisha mji mkuu kwenda Edo iliyoitwa "Tokyo" yaani "mji mkuu wa mashariki". Mji ulikuwa na tayari mwishoni mwa karne ya 19 ulikuwa mji mkubwa wa pili duniani baada ya London.

Tokyo iliharibiwa na moto katika historia yake, pia na matetemeko ya ardhi na mabomu wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ilijengwa upya na kukua kuwa jiji kubwa duniani.

Ilikuwa mahali pa michezo ya Olimpiki ya mwaka 1964.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Japani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tokyo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.