Tenno

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tenno Naruhito.

Tenno ni cheo cha mfalme au kaisari wa Japani. Kufuatana na katiba ya nchi yeye ni "ishara wa dola na wa umoja wa taifa".

Tenno wa sasa ni Naruhito (tangu mwaka 2019, alipomrithi baba yake).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Historia ya Japani inamkumbuka tenno wa kwanza kabisa aliyekuwa Jimmu mnamo 660 KK. Wataalamu wengine huwa na shaka lakini wanakubali ya kwamba watawala hao walikuwepo angalau tangu karne ya 5 BK. Hadi karne ya 19 ikulu yao ilikuwa mjini Kyoto, lakini tangu Meiji iko Tokyo.

Nasaba ya watawala wa Japani ni nasaba ya kale zaidi duniani.

Katika historia hiyo ndefu matenno walikuwa na madaraka tofautitofauti. Hata kama walitazamwa kama wakuu wa taifa hali halisi madaraka yao yalikuwa madogo wakati mwingine. Lakini kulikuwa pia na matenno walioamua kabisa juu ya siasa ya nchi kwa mfano Meiji tangu mwaka 1868.