Salvio wa Albi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wat. Gregori na Salvio mbele ya mfalme Kilperiki I (mchoro mdogo wa karne ya 14).

Salvio wa Albi (alifariki Albi, Aquitania, leo nchini Ufaransa, 10 Septemba 584) alikuwa kwanza mwanasheria, halafu mmonaki aliyelazimishwa kuwa askofu wa mji huo[1].

Baada ya kupewa daraja takatifu hiyo mwaka 574 hakuacha kundi lake hata baada ya njaa na tauni kulipata. Ugonjwa huo ndio uliomuua[2].

Ndugu yake wa mbali, Gregori wa Tours, aliandika habari za maisha yake[3] .

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Clément Compayré, Études historiques et documents inédits sur l'Albigeois, le Castrais, et l'ancien diocèse de Lavaur (Albi, 1841)
  2. [1]
  3. Gregory of Tours, Historia Francorum, Book V, 44 and 50; Book VI, 29; Book VII, 1; and Book VIII, 22
  4. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.