Popo-wadudu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Popo-wadudu
Popo pua-njumufarasi mdogo (Rhinolophus hipposideros)
Popo pua-njumufarasi mdogo
(Rhinolophus hipposideros)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Ngeli ya chini: Eutheria
Oda: Chiroptera (Popo)
Nusuoda: Yangochiroptera (Popo-wadudu)
Koopman, 1985
Ngazi za chini

Familia 14:

Popo-wadudu ni aina za popo wanaowinda wadudu hasa. Kibiolojia ni mamalia wa nusuoda Yangochiroptera katika oda Chiroptera wanaofanana na panya wenye mabawa. Kwa kawaida spishi hizi ni ndogo kuliko zile za nusuoda Yinpterochiroptera (popo-matunda) lakini kuna spishi zilizo kubwa kulika spishi fulani za popo-matunda. Spishi ndogo kabisa ni popo nyukibambi aliye na urefu wa mm 29-33 na uzito wa g 2. Kwa hivyo popo huyu ni spishi ndogo kabisa ya mamalia pia. Kirukanjia wa Etruski anaweza kuwa na uzito mdogo zaidi (g 1.2-2.7) lakini ni mrefu zaidi (mm 36-53). Popo-wadudu hula wadudu hasa lakini spishi nyingine hula samaki, ndege na wanyama wadogo na hata damu. Hutumia miwangwi ya sauti yao ili kuyakamata mawindo yao. Spishi kadhaa hula matunda na mbochi na hizi hazitumii miwangwi.

Mwainisho[1][hariri | hariri chanzo]

Oda: Chiroptera

Picha[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. James M. Hutcheon and John A.W. Kirsch (2006). "A moveable face: deconstructing the Microchiroptera and a new classification of extant bats". Acta Chiropterologica 8: 1–10. doi:10.3161/1733-5329(2006)8[1:AMFDTM]2.0.CO;2.