Pere Ermengol

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa Vicente Carducho ukionyesha Mt. Petro Ermengol alivyookolewa na Bikira Maria baada ya kunyongwa.

Pere Ermengol, O. de M. (1238 hivi – 27 Aprili 1304) alikuwa mtawa wa Kanisa Katoliki kutoka Tarragona, Catalonia, Hispania ambaye alikwenda Algeria na Moroko kukomboa watumwa akanyongwa kwa ajili ya imani yake asife.

Kabla ya hapo aliwahi kuongoza kikosi cha majambazi, lakini baada ya kuongoka alijiunga na Shirika la Bikira Maria wa Mersede na kujitosa katika utekelezaji wa karama yake bila kujali hatari kwa uhai wake[1].

Papa Inosenti XI alimtangaza mwenye heri 28 Machi 1686 halafu mtakatifu tarehe 8 Aprili 1687.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 27 Aprili[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.