Mlei

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mlei mwanamke akisoma Biblia.

Mlei ni jina la kisheria la Mkristo wa kawaida, yaani yule asiye na daraja takatifu wala si mtawa.

Jina hilo linatokana na neno la Kigiriki λαϊκός (laikós, "mmoja wa umma"), ambalo shina lake ni λαός (laós, "umma").

Msingi wa hadhi, wajibu na haki zake ni sakramenti ya Ubatizo pamoja na Kipaimara na Ekaristi.

Mtaguso wa pili wa Vatikano ulitoa hati maalumu kuhusu utume wa walei, "Apostolicam Actuositatem".

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mlei kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Alexandre Faivre, Chrétiens et Églises : des identités en construction. Acteurs, structures, frontières du champ religieux chrétien, Paris, Cerf-Histoire, 2011, (klèros/laïkos. Deux ensembles flous à l'origine d'une dichotomie mutuellement exclusive, p. 243-311)