Milele

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Milele ni neno linalomaanisha uwepo usio na mwanzo wala mwisho unavyosadikiwa na dini mbalimbali kuhusu Mungu.

Wazo hilo gumu kufikiriwa linapingana na lile la muda ambalo linaeleweka kirahisi kwa sababu binadamu amezoea mfululizo wa nyakati, kama vile jana, leo na kesho.

Kama vile muda unavyoendana na mabadiliko, milele ni hali isiyokubali badiliko lolote, kutokana na ukamilifu wake.

Ni maarufu ufafanuzi wake uliotolewa na Severino Boesyo kwa Kilatini: "Interminabilis vitae tota simul et perfecta possessio" (Consolatio Philosophiae, V, vi). Tafsiri yake ni: "Uzima usio na mwisho unaomilikiwa wote pamoja na kikamilifu".

Ishara[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.