Maginetiti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Maginetiti kutoka Afrika Kusini

Maginetiti ni madini yenye rangi nyeusi-kijivu yenye tabia ya sumaku. Kikemia ni oksidi ya feri (chuma) yenye valensi za 2+ na 3+. Fomula yake ni Fe3+2Fe2+O4.

Inatokea mara nyingi kwa umbo la fuwele zenye urefu wa karibu sentimita 1 na kona 8. Kiwango cha feri (chuma) hufikia asilimia 72 kwa hiyo ni malighafi muhimu kwa kutengeneza chuma.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Maginetiti kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.