Machakos

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Machakos, Kenya


Machakos
Machakos is located in Kenya
Machakos
Machakos

Mahali pa mji wa Machakos katika Kenya

Majiranukta: 1°31′0″S 37°16′0″E / 1.51667°S 37.26667°E / -1.51667; 37.26667
Nchi Kenya
Kaunti za Kenya Machakos
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 150,041

Machakos ni mji wa Kenya (Ukambani) takriban kilomita 64 upande wa kusini-mashariki wa Nairobi. Ni makao makuu ya kaunti ya Machakos.

Machakos imekua haraka kwa sababu ni karibu na mji mkuu wa taifa imeshapita idadi ya wakazi lakhi moja na nusu[1]. Wenyeji wa Machakos ni hasa Wakamba.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Machakos ni kati ya miji ya kwanza ya Kenya bara ikaundwa mwaka 1899 na Waingereza na kuwa makao makuu ya koloni la Afrika ya Mashariki ya Kiingereza (mbali na eneo lindwa la pwani lililokodishwa na Usultani wa Zanzibar na Uingereza) kwa muda mfupi.

Jina la mji lilitokana na chifu Masaku wa Wakamba aliyewahi kuwa na boma lake hapo.

Baada ya azimio la kutounganisha Machakos na reli ya Uganda mji haukuendelea sana.

Mwaka 2002 majadiliano kati ya pande mbalimbali za vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Sudan yalifanyika Machakos.

Kituo kikuu cha mabasi mjini Nairobi huitwa na wenyeji "Machakos Country Bus".

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]