Guinea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Gine
République de Guinée (Kifaransa)
Hawtaandi Gine (Kipular)
ߖߌ߬ߣߍ߫ ߞߊ ߝߊߛߏߖߊߡߊߣߊ (Kimaninka)
Kaulimbiu ya taifa:
Travail, Justice, Solidarité (Kifaransa)
"Kazi, Haki, Mshikamano"
Wimbo wa taifa: Liberté (Kifaransa)
"Uhuru"
Mahali pa Guinea
Mahali pa Guinea
Ramani ya Guinea
Ramani ya Guinea
Mji mkuu
na mkubwa nchini
Conakry
9°31′ N 13°42′ W
Lugha rasmiKifaransa
Lugha za kawaidaKupita lugha 40

Gine, (pia: Gini; Kifaransa: Guinée; Kiingereza: Guinea) kirasmi Jamhuri ya Gine, ni nchi katika Afrika ya Magharibi. Pengine inatajwa kama Gine-Conakry ili kuitofautisha na nchi za Gine-Bisau na Gine ya Ikweta.

Imepakana na Gine-Bisau, Senegal na Mali upande wa kaskazini, Kodivaa, Liberia na Sierra Leone kusini halafu Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi.

Eneo lake ni chanzo ya mito mikubwa ya Niger, Senegal na Gambia.

Jina[hariri | hariri chanzo]

Jina la "Gine" liliwahi kutaja sehemu kubwa ya Afrika ya Magharibi kati ya jangwa la Sahara na Ghuba ya Gine ya Atlantiki likimaanisha "nchi ya watu weusi" kwa lugha ya Kiberberi.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Makabila yaliyopo nchini ni 24. Kubwa zaidi ni lile la Wafulani (40%).

Lugha rasmi ni Kifaransa, lakini wakazi wanatumia zaidi lugha asilia kadiri ya makabila, hasa Kipular, Kimaninka, Kisusu, Kikisi, Kikpelle na Kiloma,

Upande wa dini, 85% ni Waislamu (hasa Wasuni), 8% ni Wakristo (hasa Wakatoliki) na 7% ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Serikali[hariri | hariri chanzo]

Habari[hariri | hariri chanzo]

Muziki[hariri | hariri chanzo]

Orodha[hariri | hariri chanzo]


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guinea kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.