Ghorofa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mpango wa ghorofa

Ghorofa ni jengo la ngazi ambalo linaweza kutumiwa na watu (kwa ajili ya maisha, kazi, ghala, burudani, n.k.). 

Sakafu inayogusana na ardhi huitwa "ghorofa la chini" katika maeneo mengi.[1] 

Maelezo

Majengo ya kawaida huwa sakafu moja au mbili tu. Jengo refu zaidi katika dunia, Burj Khalifa, lina sakafu 163.

Urefu wa kila ghorofa hulingana na urefu wa dari za vyumba pamoja na unene wa sakafu kati ya kila dirisha. Maghorofa ndani ya jengo hayana haja ya kuwa na urefu mmoja.

Kuna maegesho ya magari yaliyo ya ghorofa, hujulikana pia kama gereji la kuegeshea, na hata mashamba ya Mungu ya maghorofa.

Jinsi ya kuhesabu

Nambari ya ghorofa huhesabiwa kutumia mfumo wa kuhesabu ghorofa.

  • Mfumo mmoja mkuu ni ule unaotumika Ulaya pamoja na Uhindi na nchi kadhaa zilizokuwa koloni za Uingereza au Ufaransa ambao huhesabu sakafu ya chini (inayogusa ardhi) kama nambari 0 au 'G' (ground floor) na sakafu zilizo juu yake kuhesabiwa kutoka nambari 1 kwenda juu.
  • Ule mwingine unatumika Marekani, Kanada na sehemu za Asia ambapo huhesabu nambari ya sakafu kutoka inayogusa ardhi.[2]

Vitufe vya Lifti

Vitufe vya lifti

Katika Kenya, na maeneo yanayotumia mfumo wa Uropa, lebo ya kitufe cha sakafu ya chini huwa 'G'. Sakafu zinazofuata huhesabu nambari 1 na kuendelea. Sakafu zilizo chini ya ardhi huhesabu kutoka B1 kuendelea unavyoshuka.

Angalia pia

Marejeo

  1. "Story | Define Story at Dictionary.com". Dictionary.reference.com. 
  2. "Rick Steves' Europe through the back door 2011". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2014-04-22. Iliwekwa mnamo 2017-12-02. 
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.