Ghala

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ghala linalohifadhi vipuri vidogo

Ghala ni jengo linalohifadhi bidhaa kama vile malighafi, vipuri, au bidhaa zinazohusiana na kilimo, viwanda na uzalishaji.

Ghala hutumiwa na wazalishaji, waagizaji, wauzaji wa nje, wauzaji wa jumla, wafanya biashara za usafiri, forodha, n.k.

Kwa kawaida huwa majengo makuu makubwa katika maeneo ya viwanda ya mijini na vijijini.

Mara nyingi huwa na sehemu maalum ya kupakia na kupakua bidhaa kutoka kwenye malori. Wakati mwingine ghala hujengwa kwa ajili ya upakiaji na upakuaji bidhaa wa moja kwa moja kutoka kwenye reli, viwanja vya ndege, au bandari.

Mara nyingi huwa na kambarau kwa ajili ya kunyanyua bidhaa.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ghala kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.