Frigia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani inayoonyesha Frigia katika rasi ya Anatolia.

Frigia (kwa Kiing. Phrygia) ni jina la ufalme wa zamani, halafu mkoa wa milki mbalimbali zilizotawala Anatolia ambayo leo hii inaunda sehemu kubwa ya nchi ya Uturuki.

Kati ya wafalme mashuhuri wa Frigia alikuwepo Midas anayekumbukwa kama tajiri kwa sababu inasimuliwa kwamba kila kitu alichokigusa kilibadilika kuwa dhahabu.

Mji mkuu wa Frigia ilikuwa Gordion; mabaki yake yamegunduliwa na wanaakiolojia karibu na mji wa Eskishehir. Aleksander Mashuhuri alipita huko akakuta "fundo la Gordion" lililofanywa na kamba la kushika gari kwenye hekalu la mji; kulikuwa na utabiri uliosema "atakayefungua fundo hilo atatawala Asia". Aleksander alipopita akaangalia fundo akatoa upanga wake na kukata fundo.

Wakazi walioitwa Wafrigia walitokea Ulaya na kuzungumza lugha iliyofanana kidogo na Kigiriki.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.