Faida

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Faida ni neno linalotumika baada ya matokeo yanayohushisha mchakato fulani ambao umetokea kwa lengo fulani na kusababisha matokeo yenye mtazamo chanya.

Mara nyingi neno faida hutumika biashara baada ya tuweza kusababisha ongezezo la mtaji baada ya uzalishaji kwa sababu mara zote lengo kuu la kufanya biashara ni kupata faida.

Lakini pia katika maisha ya kila siku mashuleni, nyumbani neno faida hutumika. Hii hutokea baada ya kuonyesha jambo zuri ambalo litafurahisha watu katika jamii yako mfano mtu huweza kusema: "Kuna faida kubwa sana ya kupata elimu" au "Usipokuwa mtoto msikivu utaiona faida yake!".

Hivyo neno faida katika maisha ya kila siku halikwepeki kutumika kwani ni la kawaida na hutumika mara nyingi sana.