Bahari ya Maluku

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Bahari ya Maluku.
Bahari ya Maluku.

Bahari ya Maluku (kwa Kiingereza: Moluccan Sea) ni sehemu ya Bahari ya Pasifiki, ndani ya nchi ya Indonesia. Ni eneo lenye miamba tumbawe mingi na nafasi nzuri ya kupiga mbizi.

Bahari ya Maluku inapakana na Bahari ya Banda upande wa kusini na Bahari ya Celebes upande wa kaskazini.

Iko kati ya visiwa vya Maluku na Sulawesi (Celebes). Visiwa vya Talaud kaskazini ndivyo mwisho wa bahari hiyo.

Eneo lake ni takriban kilomita za mraba 200,000. Kina cha maji hufikia mita 4,810.

Chini ya bahari hii mabamba ya gandunia husukumana na hivyo kusababisha matetemeko ya ardhi ya mara kwa mara.

Tovuti za Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bahari ya Maluku kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.