Antonino Fantosati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha yake halisi.

Antonino Fantosati (Trevi, Umbria, Italia, 16 Oktoba 1842 - Taiyuan, Shanxi, China, 7 Julai 1900) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo na askofu mmisionari wa Kanisa Katoliki aliyeuawa kwa kupigwa mawe huku akijitokeza pamoja na padri Yosefu Maria Gambaro kutetea waumini wakati wa Uasi wa Waboksa nchini China[1].

Alitangazwa na Papa Pius XII kuwa mwenye heri tarehe 27 Novemba 1946.

Anaheshimiwa na Kanisa hilo kama mtakatifu mfiadini tangu tarehe 1 Oktoba 2000, alipotangazwa na Papa Yohane Paulo II pamoja na wenzake 119 maarufu kama wafiadini wa China.

Sikukuu yao huadhimishwa kwa pamoja kila mwaka tarehe 9 Julai, lakini ya kwake mwenyewe tarehe ya kifodini chake[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/91735
  2. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.