Masafa ya mawimbi : Tofauti kati ya masahihisho
No edit summary |
d Kipala alihamisha ukurasa wa Urefu wa wimbi hadi Masafa ya mawimbi |
(Hakuna tofauti)
|
Pitio la 14:39, 28 Aprili 2017
Urefu wa wimbi (pia masafa[1], mara chache lukoka[2]; kwa Kiingereza wavelength) ni namna ya kupima na kutaja ukubwa wa wimbi.
Ni umbali kati ya sehemu za kulingana za mawimbi mawili ambayo yanafuatana, kwa mfano kati ya kilele na kilele au mabonde yao.
Mawimbi yapo kila sehemu ya mazingira asilia, kwa mfano:
- mawimbi ya maji
- mawimbisauti
- mawimbi sumakuumeme pamoja na nuru na wimbiredio
Urefu wa mawimbi unatofautiana sana. Mawimbi marefu yanayoweza kutambuliwa na milango ya fahamu ya binadamu ni sauti ya besi yenye lukoka ya mita 21. Sikio letu linatambua mawimbi yenye urefu kati ya milimita 17 hadi mita 21.
Mawimbi sumakuumeme yana upeo mkubwa.
- Urefu wa wimbiredio ni kati ya milimita 1 hadi kilomita 100.
- nuru inayoonekana kwa macho yetu ina lukoka kati ya nanomita 380 (urujuani) hadi 780 (nyekundu). Nyuki huona pia mnururisho mfupi zaidi yaani urujuanimno, lakini hawaoni nyekundu.
- eksirei zina lukoka baina ya nanomita 0.01 hadi 10.
- urefu wa mawimbi gammarei iko katika upeo wa pikomita.
Urefu wa wimbi na marudio
Urefu wa wimbi huwa na uhusiano wa kinyume na marudio ya wimbi. Kama marudio ya wimbi ni ya juu, urefu wake ni mdogo. Vilevile kinyume, kama wimbi lina urefu mkubwa, marudio yake ni madogo.