Kitenzi : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
No edit summary
Mstari 1: Mstari 1:
Na EMANUEL GASPA KAWISHE. {{ExamplesSidebar|35%|
{{ExamplesSidebar|35%|
*''''Anacheza''' muziki
*''''Anacheza''' muziki
*'''Wanaenda''' kazini
*'''Wanaenda''' kazini

Pitio la 09:01, 27 Novemba 2016

Mifano
  • 'Anacheza muziki
  • Wanaenda kazini
  • Unaimba wimbo wa taifa
  • Ninasema Kifaransa

Kitenzi ni istalihi ya sarufi kwa maneno yanaotaja matendo kama vile kufanya, kwenda, kulala, kupiga, kuishi na kadhalika.

Lugha nyingi zinatumia vitenzi ingawa kuna pia lugha zisizoweka tofauti kati ya vitenzi na majina.

Maumbo ya kitenzi

Kwa Kiswahili kila kitenzi kina shina yake inayobeba maana yake. Mfano: ku-fanya ambamo "fanya" ni shina; kiambishi awali "ku-" ni alama ya aina ya neno yaani kitenzi chenyewe.

Ndani ya shina kuna tofauti kati ya mzizi wa neno "fany" na kiambishi tamati ambacho ni silabi "a".

Mzizi wda kitenzi mwenyewe haubadiliki wakati wowote kitenzi kitaponyambuliwa katika kauli yoyote iwayo.

Vitenzi kwa Kiswahili hupokea viambishi mbalimbali vinavyoeleza kwa undani zaidi maana ya matumizi ya neno. Viambishi awali ni silabi zilizopo mbele ya mzizi na viambishi tamati ni silabi zilivyopo baada ya mzizi wa kitenzi.

Viambishi awali vinaweza kutaja:

  • nafsi ya mtenda - ni nani au nani anayetenda na hivi ni silabi ni /u / a upande wa umoja na tu / m / wa upande wa uwingi mtawalia katika hali yakinishi na "si"/ "hu"/"ha" kuwa vikanushi vya viambishi vya nafsi za mtenda- umoja na "hatu"/"ham"/"hawa" kuwa vikanushi vya viambishi vya nafsi za mtenda-wingi .
  • njeo au wakati - kama tendo linatokea sasa au lilitokea wakati uliopita au litatokea wakati ujao ; mifano ni silabi za a pamoja na na kwa wakati wa kisasa, li kwa wakati uliopita na ta kwa wakati ujao katika hali yakinishi.

Viambishi tamani vinaweza kupanusha au kubadilisha maana ya kimsingi ya mzizi wa neno. Mifano ni kimbi-a, kimbi-lia, kimbili-ana, kimbi-za, kimbi-zana, kimbi-liwa.

Kwa jumla kitenzi cha Kiswahili kinaweza kuwa na sehemu saba yaani shina na hadi sita viambishi mbele au nyuma ya shina la neno. Jedwali inayofuata inaonyesha mifano kadhaa. Umbo fupi zaidi ya kitenzi ni amri kama "piga".

Kitenzi cha Kiswahili
pamoja na viambishi vyake
1 2 3 4 5 6 7
Viambishi awali Shina Viambishi tamati
Viambishi vya
Nafsi Mtenda
Viambishi vya
Wakati / Hali
Viambishi
Virejeshi
Viambishi vya
Nafsi Mtendewa
Viambishi vya
Kauli
Kiishio
ni na - - sem - a
u me ni on yesh a
a na cho ni ambi - a
tu li po wa ingi z a
pig - a

Aina za vitenzi

Tazama pia

Marejeo

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitenzi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.