Burundi : Tofauti kati ya masahihisho
historia |
|||
Mstari 81: | Mstari 81: | ||
== Historia == |
== Historia == |
||
===Ufalme wa Burundi== |
|||
Dola la kwanza katika eneo hili lilikuwa Ufalme wa Burundi. Katika mapokeo ya wenyeji ulianzishwa katika karne ya 17 na mtu kwa jina la Cambarantama aliyefika ama kutoka Rwanda au kutoka Buha katika [[Mkoa wa Kigoma]], Tanzania ya leo. |
Dola la kwanza katika eneo hili lilikuwa Ufalme wa Burundi. Katika mapokeo ya wenyeji ulianzishwa katika karne ya 17 na mtu kwa jina la Cambarantama aliyefika ama kutoka Rwanda au kutoka Buha katika [[Mkoa wa Kigoma]], Tanzania ya leo. |
||
Mstari 87: | Mstari 88: | ||
Ufalme huu ulienea katika karne zilizofuata. Mwami Ntare IV Rutaganzwa Rugamba aliyetawala mnamo 1796 hadi 1850 aliweza kupanusha mipaka ya ufalme wake hadi kushika sehemu kubwa ya eno la leo. |
Ufalme huu ulienea katika karne zilizofuata. Mwami Ntare IV Rutaganzwa Rugamba aliyetawala mnamo 1796 hadi 1850 aliweza kupanusha mipaka ya ufalme wake hadi kushika sehemu kubwa ya eno la leo. |
||
===Ukoloni=== |
|||
Wazungu wa kwanza waliofika walikuwa wapelelezi Waingereza [[Richard Burton]] and [[John Hanning Speke]] mnamo mwaka 1854. Walifuatwa na wengine na 1894 Mjerumani wa kwanza alipita hapa aliyekuwa [[Oskar Baumann.]] Wakati ule Ujerumani uliwahi tayari kuanzisha koloni yake ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini Wajerumani walichelewa kufika kwenye kaskazini-magharibi ya maeneo waliyotazama kuwa sehemu yao. Katika Burundi kikosi cha kwanza cha Kijerumani kilifika mnamo 1896 wakakuta ufalme wa mwami wakaridhika kumwacha mwakilishi mkazi (resident) |
Wazungu wa kwanza waliofika walikuwa wapelelezi Waingereza [[Richard Burton]] and [[John Hanning Speke]] mnamo mwaka 1854. Walifuatwa na wengine na 1894 Mjerumani wa kwanza alipita hapa aliyekuwa [[Oskar Baumann.]] Wakati ule Ujerumani uliwahi tayari kuanzisha koloni yake ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini Wajerumani walichelewa kufika kwenye kaskazini-magharibi ya maeneo waliyotazama kuwa sehemu yao. Katika Burundi kikosi cha kwanza cha Kijerumani kilifika mnamo 1896 wakakuta ufalme wa mwami wakaridhika kumwacha mwakilishi mkazi (resident) katika mji mkuu [[Gitega]] ambaye hakuhusika na mambo ya utwala wa ndani. Wakati ule eneo lilijulikana kwa jina "Urundi". Hapa sawa na Rwanda na Bukoba Wajerumani walitumia mbinu wa [[eneo lindwa]] ingawa vyanzo wa nyakati zile zinaonyesha ya kwamba walikuwa pia na majadiliano kuingiza falme hizi za kienyeji moja kwa moja ndani ya koloni yao. |
||
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Burundi pamoja na Rwanda ilikabidhiwa kwa Ubelgiji kwa niaba ya [[Shirikisho kwa Mataifa]]. Kimsingi Wabelgiji waliendelea na mfumo wa Wajerumani uliomwacha mtemi mamlaka makubwa. |
|||
== Utawala == |
== Utawala == |
Pitio la 11:41, 9 Mei 2015
Burundi |
---|
Jamhuri ya Burundi (iliyojulikana zamani kama Urundi) ni nchi ndogo ambayo iko katika eneo la Maziwa Makubwa ya Afrika. Burundi imepakana na Rwanda upande wa kaskazini, Tanzania upande wa mashariki, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa magharibi.
Jina lenyewe la nchi hii, limetokana kwa msingi na kutanuka kwa lugha ya Kirundi ambacho ni lugha ya Kibantu.
Jiografia
Burundi ni kati ya nchi ndogo zaidi zilizomo barani Afrika. Wakazi milioni 10 ni wengi kulingana na eneo dogo la nchi, msongamano wa watu ni wakazi 379 kwenye kila kilomita ya mraba.
Ingawa Burundi haina bahari, sehemu ya mpaka wake eneo la mashariki unaishia kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika.
Eneo lote ni nyanda za juu zenye kimo cha mita 1700 juu ya UB kwa wastani. Sehemu ya juu zaidi ni kilele cha mlima Heha chenye mita 2685 juu ya uwiano wa bahari uliopo katika safu ya milima inayopakana na bonde la ufa la Afrika ya Mashariki.
Sehemu ya magharibi ya nchi ni sehemu ya bonde la ufa yenye kimo cha mita 760-850 juu ya uwiano wa bahari. Sehemu ya kusini ya bonde la ufa katika Burundi imejaa maji ya Ziwa Tanganyika.
Upande wa mashariki wa safu ya milima inayopakana na bonde la ufa kuna chanzo cha mto Ruvyironza (pia: Luvironza) unaoishia katika mto Kagera na hivyo huhesabiwa kati ya vyanzo vya mto Naili.[1]
Hali ya hewa ni ya kitropiki: kuna vipindi viwili vya mvua. Joto linapungua kutokana na kimo cha nchi. Kuna mvua kwa wastani wa milimita 1,000 kwa mwaka.
Matumizi ya ardhi ni kwa ajili ya kilimo au mifugo. Msongamano wa watu umesababisha kuenea kwa ukataji wa misitu, mmomonyoko wa ardhi na kupotea kwa ardhi yenye rutuba[2]. Eneo la misitu lililobaki ni kilomita cha mraba 600 pekee linalopungua kwa kasi ya asilimia 9 kwa mwaka[3].
Kuna hifadhi mbili za taifa ambazo ni Hifadhi ya Taifa ya Kibira kwenye kaskazini-magharibi (inapakana na Msitu wa Nyungwe huko Rwanda), na Hifadhi ya Taifa ya Ruvubu upande wa kaskazni-mashariki karibu na mto Rurubu (pia Ruvubu au Ruvuvu). Hifadhi zote mbili zilianzishwa mwaka 1982 kwa shabaha ya kuhifadhi wanyamapori[4].
Hali ya nchi kijamii na kisiasa
Mara kadhaa nchi hii imekuwa na misukosuko na machafuko ya kisiasa na ya kijamii. Shida kubwa ni kuwa Burundi haina maliasili ya kutosheleza umma na kutosheleza ratili ya kisiasa kwa walio wengi Wahutu na walio wachache Watutsi na Watwa. Pia kuna kabila la Warundi wanaojinasibu kuwa wao sio Watutsi wala Wahutu bali ni Waswahili. Hilo kabila la Waswahili lilikuwepo toka enzi za tawala za kifalme nchini humo, na ndio wenyeji wa jiji la Bujumbura, waliomsaidia Mwanamfalme Louis Rwagasore katika harakati za kutafuta uhuru wa Burundi.
Historia
=Ufalme wa Burundi
Dola la kwanza katika eneo hili lilikuwa Ufalme wa Burundi. Katika mapokeo ya wenyeji ulianzishwa katika karne ya 17 na mtu kwa jina la Cambarantama aliyefika ama kutoka Rwanda au kutoka Buha katika Mkoa wa Kigoma, Tanzania ya leo.
Ufalme huu ulitawaliwa na kundi la Watutsi waliokuwa wafugaji wa ng'ombe na kutawala wenyeji waliokuwa wakulima Wabantu. Watutsi walikuwa takaba la kikabaila. Mfalme au mwami alikuwa mkuu wa makabaila hawa ambao walitazamiwa kama mabwana wa ardhi iliyolimwa na watu wa kawaida. Hao wakulima waliruhusiwa kulima nchi wakipaswa kutoa huduma na sehemu ya mavuno kwa mabwana waliopaswa kuwatetea dhidi maadui.
Ufalme huu ulienea katika karne zilizofuata. Mwami Ntare IV Rutaganzwa Rugamba aliyetawala mnamo 1796 hadi 1850 aliweza kupanusha mipaka ya ufalme wake hadi kushika sehemu kubwa ya eno la leo.
Ukoloni
Wazungu wa kwanza waliofika walikuwa wapelelezi Waingereza Richard Burton and John Hanning Speke mnamo mwaka 1854. Walifuatwa na wengine na 1894 Mjerumani wa kwanza alipita hapa aliyekuwa Oskar Baumann. Wakati ule Ujerumani uliwahi tayari kuanzisha koloni yake ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini Wajerumani walichelewa kufika kwenye kaskazini-magharibi ya maeneo waliyotazama kuwa sehemu yao. Katika Burundi kikosi cha kwanza cha Kijerumani kilifika mnamo 1896 wakakuta ufalme wa mwami wakaridhika kumwacha mwakilishi mkazi (resident) katika mji mkuu Gitega ambaye hakuhusika na mambo ya utwala wa ndani. Wakati ule eneo lilijulikana kwa jina "Urundi". Hapa sawa na Rwanda na Bukoba Wajerumani walitumia mbinu wa eneo lindwa ingawa vyanzo wa nyakati zile zinaonyesha ya kwamba walikuwa pia na majadiliano kuingiza falme hizi za kienyeji moja kwa moja ndani ya koloni yao.
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Burundi pamoja na Rwanda ilikabidhiwa kwa Ubelgiji kwa niaba ya Shirikisho kwa Mataifa. Kimsingi Wabelgiji waliendelea na mfumo wa Wajerumani uliomwacha mtemi mamlaka makubwa.
Utawala
Burundi imegawiwa katika mikoa 18 (kwa Kifaransa province, kwa Kirundi: IProvense) inayoitwa kufuatana na miji yenye makao makuu ya utawala.
*Angalia Mikoa ya Burundi
Mikoa imegawiwa kwa wilaya inayoitwa "communes" na hii imegawiwa kwa "collines" (vilima).
Watu na Utamaduni
Utafiti
Mambo mengi ya Burundi yamepatikana kutoka CIA World Factbook 2000 na 2003 U.S. Department of State website.
Kichunguzi
Ongezea masomo kwa wingi
- Burundi: Ethnic Conflict and Genocide Reni Lemarchand and Lee H. Hamilton
Tazama pia
Tanbihi
- ↑ [Klohn, Wulf and Mihailo Andjelic. [http://www.fao.org/ag/AGL/AGLW/webpub/lakevic/LAKEVIC4.htm Lake Victoria: A Case in International Cooperation]. Food and Agriculture Organization of the United Nations. Retrieved on July 20, 2008]
- ↑ [Bermingham, Eldredge, Dick, Christopher W. and Moritz, Craig (2005). ''Tropical Rainforests: Past, Present, and Future''. Chicago, Illinois: [[University of Chicago]] Press, p. 146. ISBN 0-226-04468-8]
- ↑ [http://www.mongabay.com/deforestation.htm Worldwide Deforestation Rates] Food and Agriculture Organization of the U.N.: The State of the World's Forests 2003. Published on Mongabay.com. Retrieved on June 29, 2008.
- ↑ East, Rob (1999). ''African Antelope Database 1998''. [[Gland, Switzerland]]: [[International Union for Conservation of Nature]], p. 74. ISBN 2-8317-0477-4.
Viungo vya nje
Serikali
- (Kifaransa) Tovuti ya serikali ya Burundi
Habari
- (Kifaransa) Agence Burundaise de Presse (ABP)
- Habari za Burundi toka tovuti ya habari ya allAfrica - Burundi
- Radio Isanganiro Radio binafsi nchini Burundi kwa Kifaransa na Kirundi na Kiswahili.
- umuco.com Habari kuhusu Burundi kwa Kifaransa
- (Kiingereza) (Kifaransa) Burundi Réalités Habari na Uchambuzi kwa Kiingerenza na Kifaransa.
Overviews
Maendelezo
- Open Directory Project - Burundi directory category
- Stanford University - Africa South of the Sahara: Burundi directory category
- University of Pennsylvania - African Studies Center: Burundi directory category
- Yahoo! - Burundi directory category
Vinginevyo
- Burundian Human Rights Organisation "Ligue Iteka" - with up-to-date news in English and French
- Campaign for the prosecution of FNL leader Agathon Rwasa
- Human Rights Watch reports on Burundi
- Woodrow Wilson Center Reports on Burundi
- Human Rights Watch special report on the August 2004 Gatumba massacre
- Links to political analyses from 1998 on by the International Crisis Group
- Reuters Alertnet - Burundi humanitarian news
- Updated humanitarian news from the United Nations Office for the Coordination of Humanitarian Affairs
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |