Mtaguso wa tano wa Laterano : Tofauti kati ya masahihisho
+img |
+tif |
||
Mstari 1: | Mstari 1: | ||
[[File:Iulius - Bulla monitorii et declarationis in cursus privationis et aliarum penarum contra prelatos Gallice nationis hic expressos, 1511 - 4592472 BEIC3 V00109 F0055.tif|thumb|''Bulla monitorii et declarationis'']] |
[[File:Iulius - Bulla monitorii et declarationis in cursus privationis et aliarum penarum contra prelatos Gallice nationis hic expressos, 1511 - 4592472 BEIC3 V00109 F0055.tif|thumb|''Bulla monitorii et declarationis'']] |
||
[[Image:Louis - Litterae super abrogatione pragmatice sanctionis in quarta sessione sacro sancti Lateranensis concilii publice lecte et recitate, 1512 - 4592398.tif|thumb|''Litterae super abrogatione pragmatice sanctionis'', 1512]] |
|||
'''Mtaguso wa tano wa Laterano''' ulifanyika kuanzia mwaka [[1512]] hadi [[1517]] huko [[Roma]] ([[Italia]]), kwenye [[Kanisa kuu la Roma|Basilika la Mt. Yohane huko Laterano]] ambalo ndilo [[kanisa kuu]] la [[Kanisa la Roma|Jimbo Katoliki la Roma]]. |
'''Mtaguso wa tano wa Laterano''' ulifanyika kuanzia mwaka [[1512]] hadi [[1517]] huko [[Roma]] ([[Italia]]), kwenye [[Kanisa kuu la Roma|Basilika la Mt. Yohane huko Laterano]] ambalo ndilo [[kanisa kuu]] la [[Kanisa la Roma|Jimbo Katoliki la Roma]]. |
||
Pitio la 13:29, 6 Mei 2015
Mtaguso wa tano wa Laterano ulifanyika kuanzia mwaka 1512 hadi 1517 huko Roma (Italia), kwenye Basilika la Mt. Yohane huko Laterano ambalo ndilo kanisa kuu la Jimbo Katoliki la Roma.
Kanisa Katoliki linauhesabu kama mtaguso mkuu wa 18.
Uliitishwa na Papa Julius II (1503-1513) ambaye alianza kuusimamia tarehe 3 Mei 1512. Baada ya kifo chake, uliendelezwa na Papa Leo X (1513-1521) hadi kikao cha 12 na cha mwisho kilichofanyika tarehe 16 Machi 1517.
Ulihudhuriwa na maaskofu 100 hivi, wengi wao wakitokea Italia. Kutofika kwa wajumbe kutoka nchi nyingine, pamoja na wengi kukosa nia ya kujirekebisha, kulichangia kufanya utekelezaji wa maamuzi ya mtaguso ushindikane.
Maamuzi hayo yalitolewa kwa hati za Papa. Mengine yanahusu mafundisho ya imani, mengine maagizo ya urekebisho wa Kanisa.
"Kitaguso" cha Pisa
Kwa kuwa Papa Julius II alikuwa hatekelezi kiapo chake cha kuitisha mtaguso kwa ajili ya urekebisho, baadhi ya makardinali, wakihimizwa na watawala wa Ujerumani na Ufaransa, waliuitisha huko Pisa (Italia) kuanzia tarehe 1 Septemba 1511. Walikusanyika wachache tarehe 1 Oktoba, halafu katika kikao cha nane walimsimamisha Papa wakahamia Lyon (Ufaransa).
Kuitisha mtaguso
Papa aliitikia “kitaguso” hicho kwa hati ya tarehe 18 Julai 1511, ambayo pamoja na kukipinga na kujitetea aliitisha mtaguso mkuu ukusanyike tarehe 19 Aprili 1512 huko Laterano.
Mtaguso wenyewe
Vita vilichelewesha mwanzo wa mtaguso hadi tarehe 3 Mei 1512, walipokusanyika katika basilika la Laterano makardinali 15, mapatriarki 2, maaskofu wakuu 10, maaskofu 56, maabati na wakuu wa mashirika ya kitawa wachache pamoja na mabalozi wa nchi 3. Mwisho walikuwepo makardinali 23 na maaskofu 122.
Matokeo
Utekelezaji wa maagizo ya mtaguso ulikuwa mdogo sana, la sivyo pengine Matengenezo ya Kiprotestanti yasingetokea. Ukweli ni kwamba Martin Luther aliyaanzisha miezi sita tu baada ya mtaguso kwisha.