Haramia : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Addbot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 65 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q45393 (translate me)
d All info is kept in Wikidata, removed: {{Link FA|es}} (3) using AWB (10903)
Mstari 14: Mstari 14:
[[Jamii:Uharamia]]
[[Jamii:Uharamia]]
[[Jamii:Sheria]]
[[Jamii:Sheria]]
{{Link FA|es}}
{{Link FA|hr}}
{{Link FA|mk}}

Pitio la 21:38, 22 Aprili 2015

Bendera ya kihistoria ya maharamia Wazungu kwenye Atlantiki

Haramia ni jambazi anayefanya mambo yake kwenye gimba la maji hasa baharini.

Kufuatana na Mkataba wa Umoja wa Mataifa juu ya sheria za bahari uharamia ni matendo ya jinai yoyote yanayotekelezwa baharini na mabaharia au maabiria wa meli binafsi dhidi ya meli nyingine au dhidi ya watu na mali ndani yake. Kisheria matendo ya aina hii dhidi ya ndege, mizigo au maabiria zake huitwa pia uharamia.

Katika historia maharamia wamejulikana tangu habari za kwanza juu ya usafiri kwenye bahari. Kati ya habari za kwanza ni zile kuhusu maharamia kwenye Mediteranea mnamo karne ya 13 KK.

Julius Caesar alipokuwa kijana alikamatwa na maharamia akaachichwa nao baada ya malipo ya ufidiwa mkubwa lakini baadaye akarudi akalipiza kisasi na kuwaua maharamia.

Siku hizi eneo lenye uharamia mbaya ni Indonesia lakini ni hasa maharamia wa Somalia walioonekana sana katika habari tangu mwaka 2008.

Wakati mwingine maharamia walitawala pia maeneo ya mabandari walipokuwa na kimbilio chao kama dola-mji. Mfano mashuhuri wa madola haya madogo ilikuwa jamhuri ya Bou Regreg katika Moroko ya leo wakati wa karne za 17-19.