Urujuanimno : Tofauti kati ya masahihisho
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika '450px|thumbnail|Urujuanimno upande wa lukoka fupi zaidi ya spektra inayoonekana '''Urujuanimno''' (ing. ''ult...' |
+elezo fupi |
||
Mstari 1: | Mstari 1: | ||
[[Picha:Nuru inayoonekana katika spektra.jpg|450px|thumbnail|Urujuanimno upande wa lukoka fupi zaidi ya spektra inayoonekana]] |
[[Picha:Nuru inayoonekana katika spektra.jpg|450px|thumbnail|Urujuanimno upande wa lukoka fupi zaidi ya spektra inayoonekana]] |
||
'''Urujuanimno''' ([[ing.]] ''ultraviolet'', kifupi '''UV''') ni aina ya [[nuru]] isiyoonekana kwa binadamu lakini kwa wanyama mbalimbali. Kwa lugha nyingine na makini zaidi ni sehemu ya [[mnururisho wa sumakuumeme]] mwenye [[lukoka]] baina ya [[nanomita]] 400 nm hadi 10 nm, ambayo ni lukoka fupi kuliko [[urujuani]] inayoonekana lakini ndefu zaidi kuliko [[eksirei]]. |
'''Urujuanimno''' ([[ing.]] ''ultraviolet'', kifupi '''UV''') ni aina ya [[nuru]] isiyoonekana kwa binadamu lakini kwa wanyama mbalimbali. Kwa lugha nyingine na makini zaidi ni sehemu ya [[mnururisho wa sumakuumeme]] mwenye [[lukoka]] (''wavelength'') baina ya [[nanomita]] 400 nm hadi 10 nm, ambayo ni lukoka fupi kuliko [[urujuani]] inayoonekana lakini ndefu zaidi kuliko [[eksirei]]. |
||
Wanyama wengi pamoja na wadudu kadhaa, mamba, ndege wengine wadogo wanaweza kutambua urujuanimno. |
Wanyama wengi pamoja na wadudu kadhaa, mamba, ndege wengine wadogo wanaweza kutambua urujuanimno. |
Pitio la 13:57, 16 Machi 2015
Urujuanimno (ing. ultraviolet, kifupi UV) ni aina ya nuru isiyoonekana kwa binadamu lakini kwa wanyama mbalimbali. Kwa lugha nyingine na makini zaidi ni sehemu ya mnururisho wa sumakuumeme mwenye lukoka (wavelength) baina ya nanomita 400 nm hadi 10 nm, ambayo ni lukoka fupi kuliko urujuani inayoonekana lakini ndefu zaidi kuliko eksirei.
Wanyama wengi pamoja na wadudu kadhaa, mamba, ndege wengine wadogo wanaweza kutambua urujuanimno. Mnururisho wa urujuanimno unafika duniani kama sehemu ya nuru ya jua.
Mnururisho wa urujuanimno na afya ya watu
Viwango vikubwa vya mnururisho wa urujuanimno vinaweza kusababisha uharibifu kwa seli za binadamu. Ngozi ya binadamu inajenga rangi ya melanini kama kinga dhidi yake. Anga ya hewa ya dunia inachuja sehemu ya mnururisho huu lakini kwenye maeneo ya ikweta kiwango kinachopita hadi uso wa dunia ni kubwa zaidi.
Hapo ni sababu ya kwamba watu katika maeneo karibu na ikweta wana rangi nyeusinyeusi zaidi. Watu wanaoishi mbali na ikweta hawahitaji kiwango hiki cha kinga dhidi ya mnururisho wa urujuanimno na kwa sababu hiyo watu wenye rangi nyeupe zaidi waliweza kuendelea huko kaskazini. Pale ambako watu kutoka sehemu za kaskazini walihamia katika maeneo ya ikweta wana hatari kubwa zaidi kupata kansa ya ngozi na hii inaonekana katika asilimia kubwa ya kansa hii kati ya wazungu wa Australia.
Asilimia kubwa ya kansa ya ngozi kati ya watu walioathiriwa na zeruzeru katika Afrika ina sababu hiyohiyo.
Viungo vya Nje
Kujisomea
- Hu, S; Ma, F; Collado-Mesa, F; Kirsner, R. S. (July 2004). "UV radiation, latitude, and melanoma in US Hispanics and blacks". Arch. Dermatol. 140 (7): 819–824. PMID 15262692. doi:10.1001/archderm.140.7.819.
- Hockberger, Philip E. (2002). "A History of Ultraviolet Photobiology for Humans, Animals and Microorganisms" (– Scholar search). Photochemisty and Photobiology 76 (6): 561–569. PMID 12511035. doi:10.1562/0031-8655(2002)076<0561:AHOUPF>2.0.CO;2.
- Allen, Jeannie (6 September 2001). Ultraviolet Radiation: How it Affects Life on Earth. Earth Observatory. NASA, USA.