Jimbo Katoliki la Morogoro : Tofauti kati ya masahihisho
No edit summary |
kilatini >kanisa la kiroma |
||
Mstari 4: | Mstari 4: | ||
Eneo lote lina [[kilometa mraba]] 43,380. |
Eneo lote lina [[kilometa mraba]] 43,380. |
||
Kutokana na [[historia]] yake linafuata mapokeo ya [[ |
Kutokana na [[historia]] yake linafuata mapokeo ya [[Kanisa la Kiroma]], kama majimbo mengine yote ya Tanzania. |
||
==Uongozi wake== |
==Uongozi wake== |
Pitio la 08:50, 5 Januari 2015
Jimbo la Morogoro ni mojawapo katika ya majimbo 34 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania kwa ajili ya waumini wake katika manispaa ya Morogoro pamoja na wilaya za Bagamoyo, Morogoro vijijini, Mvomero, Kilosa, Gairo n.k.
Eneo lote lina kilometa mraba 43,380.
Kutokana na historia yake linafuata mapokeo ya Kanisa la Kiroma, kama majimbo mengine yote ya Tanzania.
Uongozi wake
Kwa njia ya askofu wake, Telesphore Mkude, ambaye yumo katika urika wa maaskofu unaongozwa na papa wa Roma, lina ushirika kamili na Kanisa Katoliki lote duniani.
Papa analisimamia kupitia Idara ya Uinjilishaji wa Mataifa.
Kazi zake
Likiishi katika eneo ambapo wananchi walio wengi ni Waislamu, linajadiliana nao kwa amani pamoja na kutangaza Injili ya Yesu Kristo.
Likitegemea uwezo wa Roho Mtakatifu katika liturujia linazidi kuwatakasa watu ili waishi kama watoto halisi wa Baba wa mbinguni.
Kwa mamlaka waliyokabidhiwa kwanza Mitume na kurithiwa kwa sakramenti yadaraja, linazidi kuwachunga waamini washuhudie upendo kati yao na kwa wote, hasa kwa kutumikia wanaohitaji huduma zake mbalimbali za kijamii pia (upande wa afya, elimu, n.k.).
Miundo na michango ya waamini mbalimbali
Mbali ya ofisi na taasisi mbalimbali (k.mf. seminari), miundo yake ya msingi ni parokia zilizoenea katika wilaya zake zote na zinazoongozwa na mapadri wanajimbo na wanashirika, ambao baadhi yao ni wazalendo, baadhi walitokea nchi za jirani na za mbali (hasa Asia na Ulaya).
Watawa wa kike na wa kiume wengi wa mashirika 40 hivi wanatoa mchango wa pekee kwa kushuhudia maisha ya Yesu katika useja mtakatifu, ufukara na utiifu.
Hatimaye walei, ambao ndio wanakanisa walio wengi, wanatimiza utume wao katika majukumu ya kila siku ya maisha ya kawaida vijijini na mitaani, wakishirikiana katika mtandao wa vigango, vinavyotegemea sana makatekista, na wa jumuia ndogondogo za Kikristo, zilizopewa kipaumbele na Sinodi ya Afrika.
Malengo
Ni juhudi yao kulenga hali ya kujitegemea hata kiuchumi, ingawa hali halisi ya nchi ni ngumu kwa sababu zilezile zilizoathiri karibu nchi zote za bara hilo.
Wakitegemea neema ya Mungu, ni juhudi yao hasa kushinda dhambi ndani mwao wenyewe na ndani ya miundo ya jamii ili utawala wa Mungu uenee kote na kuleta utakatifu na wokovu, haki na amani.
Takwimu
Mwishoni mwa mwaka 2007 jimbo lilikuwa na waamini waliobatizwa 645,762 kati ya wakazi 1,568,640 (41,2%).
Katika parokia 53 kulikuwa na mapadri 128 (wanajimbo 75 na watawa 53), mabradha 56 na masista 666.
Viungo vya nje
- www.catholic-hierarchy.org katika ukurasa [1]
- Giga-Catholic katika ukurasa [2]
- [3] Tovuti rasmi ya jimbo