TANZAM : Tofauti kati ya masahihisho
d Bot: Migrating 2 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q1375561 (translate me) |
No edit summary |
||
Mstari 1: | Mstari 1: | ||
[[File:T1 road sign Mikumi TZ.jpg|right|thumb|TANZAM]] |
|||
'''TANZAM''' ni kifupi cha kutaja barabara kuu ya '''Tanzania-Zambia-Highway''' kati ya [[Dar-es-Salaam]] ([[Tanzania]]) na [[Lusaka]] ([[Zambia]]). |
'''TANZAM''' ni kifupi cha kutaja barabara kuu ya '''Tanzania-Zambia-Highway''' kati ya [[Dar-es-Salaam]] ([[Tanzania]]) na [[Lusaka]] ([[Zambia]]). |
||
Pitio la 06:16, 29 Aprili 2014
TANZAM ni kifupi cha kutaja barabara kuu ya Tanzania-Zambia-Highway kati ya Dar-es-Salaam (Tanzania) na Lusaka (Zambia).
Sababu za kujengwa kwa TANZAM
Barabara hii ilipanushwa na kuimarishwa kama barabara ya lami kati ya 1968 hadi 1973. Kusudi lake lilikuwa kisiasa maana Zambia ilitafuta njia ya mawasiliano na bandari ya baharini bila kutegemea tena Afrika Kusini. Kihistoria usafiri wa nje na biashara ya Zambia isiyo na pwani zilitegemea njia zilizopita katika Msumbiji au Afrika Kusini na nchi zote mbili hazikuwa bado nchi huru. Msumbiji ilikuwa koloni ya Ureno na Afrika Kusini ilitawaliwa na serikali ya Apartheid.
Tanzania ilivutwa na mpango huu kwa sababu ilipinga ukoloni pia ilitarajia faida za biashara na Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Inchi ilkuwa pia na haja ya kuboresha barabara zake na TANZAM inaunganisha pia nyanda za juu za kusini za Tanzania na Dar es Salaam.
Tazam nadani ya Tanzania
TANZAM ina urefu wa kilomita 2,400 na zote zina lami. Katika Zambia huitwa Great North Road na ndani ya Tanzania ina namba T1.
Inaanza mjini Dar es Salaam ikipita katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Iringa na Mbeya. Kati ya Dar na Morogora njia inapita katika hifadhi ya Mikumi.
Ndani ya Tanzania ina njiapanda 4 muhimu:
- mjini Chalinze iko chanzo ya barabara kuu inayoelekea Tanga na Kilimanjaro-Nairobi
- mjini Morogoro iko njiapanda ya barabara kwenda Dodoma inayoendelea magharibi hadi Mwanza na Kigoma
- mjini Makambako kuna njiapanda ya barabara kwenda Songea inayoendelea katika hali baya hadi Mtwara
- Uyole/Mbeya iko njiapanda ya barabara kwenda Malawi kupitia Tukuyu.
Kuanzia Makambako Tanzam inaendelea mara nyingi kando la njia ya reli ya TAZARA.
Tanzam ndani ya Zambia
Mjini Tunduma Tanzam inavuka mpaka na kuingia Zambia. Sasa ni "Great North Road" ikielekea kwenda Kapiri Mposhi kupitia Nakonde na hapa inapewa namba T2. Kapiri Mposhi inajiunga na barabara kuu ya Zambia kutoka Lumbumbashi (Kongo) kwenda Lusaka.