Teresa wa Mtoto Yesu : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
Mstari 42: Mstari 42:
Mara baada ya kufa maandishi yake yalianza kusambaa kwa namna ya ajabu na kumvutia [[heshima]] ya wengi. Pia ilitokea [[miujiza]] iliyopatikana kwa maombezi yake. Ni kama alivyosema, kuwa atamimina [[mvua]] ya ma[[waridi]] kutoka [[mbinguni]], akitumia [[uzima wa milele] kutenda mema mengi duniani.
Mara baada ya kufa maandishi yake yalianza kusambaa kwa namna ya ajabu na kumvutia [[heshima]] ya wengi. Pia ilitokea [[miujiza]] iliyopatikana kwa maombezi yake. Ni kama alivyosema, kuwa atamimina [[mvua]] ya ma[[waridi]] kutoka [[mbinguni]], akitumia [[uzima wa milele] kutenda mema mengi duniani.


Mwaka [[1925]] [[Papa Pius XI]] alimtangaza mtakatifu, na mwaka [[1997]] [[Papa Yohane Paulo II]] alimtangaza mwalimu wa Kanisa kutokana na mchango wake mkubwa katika [[teolojia ya Kiroho]].
[[Papa Pius XI]] alimtangaza [[mwenye heri]] tarehe [[29 Aprili]] [[1923]], tena [[mtakatifu]] tarehe [[17 Mei]] [[1925]], na [[Papa Yohane Paulo II]] alimtangaza [[mwalimu wa Kanisa]] tarehe [[19 Oktoba]] [[1997]] kutokana na mchango wake mkubwa katika [[teolojia ya Kiroho]].


==Njia yake ya kiroho==
==Njia yake ya kiroho==

Pitio la 12:36, 15 Julai 2013

Faili:TeresadiLisieux.JPG
Picha ya Teresa akiwa amevaa kanzu na shela za Kikarmeli, 1895.

Teresa wa Mtoto Yesu na wa Uso Mtakatifu (Alençon, Ufaransa, 2 Januari 1873 - Lisieux, Ufaransa, 30 Septemba 1897) ni jina la kitawa la Thérèse Françoise Marie Martin, maarufu pia kwa jina la Teresa wa Lisieux, anayeheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu mwenye sifa za bikira na mwalimu wa Kanisa.

Tangu mwaka 1927 ni msimamizi wa wamisionari wote (pamoja na Fransisko Xavier), na tangu mwaka 1944 wa Ufaransa (pamoja na Yoana wa Arc).

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 1 Oktoba.

Maisha

Teresa mwaka 1881 akiwa na umri wa miaka 8.
Teresa muda mfupi kabla ya kusafiri kwenda Italia (1887)
Faili:Teresadarco.jpg
Teresa akiigiza kama Yoana wa Arc (1895)
Basilika la Lisieux, lenye eneo la 4500 m2 na urefu wa mita 95, lililojengwa kwa heshima yake mwaka 1937

Teresa, mtoto wa tisa na wa mwisho wa Louis Martin na Marie-Azélie Guérin (Zélie), ambao wanaheshimiwa kama wenye heri, alizaliwa tarehe 2 Januari 1873 kwenye barabara rue Saint-Blaise 42, huko Alençon (Ufaransa).

Walipokuwa vijana wazazi wake walitaka kuingia utawani, wasiweze. Baada ya kuoana, maisha yao yote yaliongozwa na imani na maadili ya Ukristo.

Teresa alipozaliwa, watoto 4 walikuwa wameshafariki.

Teresa alifiwa mama yake alipokuwa na umri wa miaka 4 tu. Hapo mjomba wake, Isidore Guerin, aliteuliwa kuwa mlezi msaidizi wa mabinti watano walioachwa na marehemu. Hivyo, tarehe 15 Novemba 1877, Louis Martin alihamia Buissonnets, kitongoji cha Lisieux, awe jirani na shemeji yake mwenye famasia. Huko Teresa alijenga uhusiano mkubwa na binamu yake Maria.

Lakini uhusiano wa pekee hasa alikuwa nao kwa dada zake Paulina na Maria, akiwaona kama mama zake.

Mwaka 1882, Paulina alipoingia monasteri ya Wakarmeli ya Lisieux, angetaka kumfuata, lakini hakuweza kutokana na umri wake mdogo. Zaidi tena alitaka kufanya hivyo Maria pia alipoingia monasteri hiyohiyo mwaka 1886.

Usiku wa Noeli iliyofuata, alishinda moja kwa moja huzuni yake iliyomfanya alielie daima. Alielewa anahitaji kumtafuta Mungu kwa ukomavu zaidi na kujipatia hivyo "elimu ya upendo".

Alipofikia umri wa miaka 14 Teresa alianza kupigania wito wake dhidi ya upinzani wa watu mbalimbali waliotaka kuahirisha hatua ya kujiunga na utawa. Kwa ajili hiyo alisafiri hadi Roma akaombe ruhusa ya Papa Leo XIII, lakini alikataliwa kwa wema. Kitu hicho kilimsikitisha lakini bila kumhangaisha, kwa sababu alijua amefanya kila aliloweza ili kuitikia wito wake mapema.

Wakati wa kurudi Ufaransa, askofu wake aliamua kubadili msimamo na kumruhusu. Hivyo tarehe 9 Aprili 1888 msichana Teresa alingiia Karmeli, akiwa na miaka 15 tu. Ile tisa iliyofuata ikawa na maendeleo ya kiroho ya kasi ajabu.

Mwaka 1893 aliteuliwa kuwa mlezi msaidizi wa wanovisi, kazi aliyofanya kwa bidii na ufanisi mkubwa. Baadaye kwa maandishi yake yaliyoenea upesi duniani kote akawa mlezi wa umati wa watu akiwaelekeza kufuata Heri Nane alizotangaza Yesu mlimani.

Mwaka 1894, baada ya ugonjwa wa muda mrefu, mzee Louis Martin alifariki, na binti yake mwingine, Selina, aliyekuwa anamtunza, aliweza kujiunga na monasteri hiyo. Kamera yake imetuachia picha halisi za Teresa.

Mwezi Aprili 1896, alipatwa na TB, ugonjwa uliokuja kumuua baada ya miezi 18. Mateso ya mwili yaliendana na yale ya ndani yanayojulikana kama "usiku wa roho".

Tarehe 10 Julai 1897 udhaifu ulimzuia asiendelee kuandika habari za maisha yake kama alivyoagizwa. Neno la mwisho aliloliandika katika sentensi isiyomalizika ni "upendo".

Alifariki tarehe 30 Septemba 1897, mnamo saa 19:20.

Heshima baada ya kufa

Mara baada ya kufa maandishi yake yalianza kusambaa kwa namna ya ajabu na kumvutia heshima ya wengi. Pia ilitokea miujiza iliyopatikana kwa maombezi yake. Ni kama alivyosema, kuwa atamimina mvua ya mawaridi kutoka mbinguni, akitumia [[uzima wa milele] kutenda mema mengi duniani.

Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri tarehe 29 Aprili 1923, tena mtakatifu tarehe 17 Mei 1925, na Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwalimu wa Kanisa tarehe 19 Oktoba 1997 kutokana na mchango wake mkubwa katika teolojia ya Kiroho.

Njia yake ya kiroho

“Njia ndogo ya utoto wa kiroho” inafundisha kutimiza sharti la Yesu: “Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia katika ufalme wa mbinguni” (Math 18:3). Njia hiyo inatia moyo wa kujitoa kikamilifu kama kikafara kwa wokovu wa ulimwengu. Mwenyewe aliifuata hata akasema: “Sijawahi kumnyima chochote Mungu mwema!”

Siri yake ni upendo, ambao Teresa alitambua ndio wito wake katika Kanisa: kuwa moyo wa Mwili wa Kristo ili kusaidia viungo vyake vyote kufanya kazi vizuri.

Sala zake

Ee Mungu wangu! Utatu mtakatifu! Natamani tu kukupenda na kukufanya upendwe...

Ili maisha yangu yaweze kuwa tendo moja tu la upendo kamili: Ninajitoa mhanga kama kitambiko cha kuteketezwa kabisa na upendo wako rahimu.

Nakusihi uniteketeze bila ya kukoma, ukiyaruhusu yale mawimbi ya upendo wako usiopimika, yanayojazana ndani yako, yafurike rohoni mwangu: hivyo nami niweze kuwa shahidi wa upendo wako, Mungu wangu!

Unijalie kifodini hicho baada ya kunitayarisha kutokea mbele yako, hatimaye unisababishe kufa: na roho yangu iruke moja kwa moja, bila ya kuchelewa popote pale, ifikie kukumbatiana milele na upendo wako rahimu.

Ee mpenzi wangu, mimi napenda, katika kila pigo la moyo wangu, kurudia upya, mara nyingi zisizohesabika, hili tendo langu la kujitoa kwako.

Mpaka hapo vivuli vitakapotoweka, nami nikaweza kukuambia milele, uso kwa uso, jinsi ninavyokupenda.


Ee Yesu, upendo wangu, hatimaye nimegundua wito wangu.

Wito wangu ni kupenda!

Ndiyo, nimeona nafasi yangu ndani ya Kanisa, na nafasi hiyo umenipatia wewe, Mungu wangu.

Katika moyo wa Kanisa, mama yangu, nitakuwa upendo: hivyo nitakuwa yote na hamu yangu itatimia.


Ee Bwana Yesu, mimi si tai, ila nina macho na moyo wake.

Ingawa ni mdogo, nathubutu kulikazia macho jua la upendo, na kutamani kurukia kwake.

Maandishi yake katika tafsiri ya Kiswahili na ya Kihaya

  • THERESIA WA MTOTO YESU, Ua la Upendo, Maisha ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu Aliyoyaandika Yeye Mwenyewe – tafsiri ya J. J. Rwechungura – ed. Paulines Publications Africa – Nairobi 1992 – ISBN 9966-21-021-0
  • THEREZA OW’OMWANA YEZU – Akamuli k’engonzi, Oburora bw’Omutakatifu Thereza Ow’omwana Yezu Obwo Yayehandikire Wenene – tafsiri ya J. J. Rwechungura – ed. Marianum Press Kisubi – Kisubi 1960

Marejeo

Viungo vya nje

Filamu juu yake

Picha zake

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.

Kigezo:Link FA