Julius Nyerere : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
No edit summary
Mstari 50: Mstari 50:
| children = 7
| children = 7
| residence =
| residence =
| alma_mater = [[Makerere University]] <small>([[Diploma of Education|DipEd]])</small> <br> [[University of Edinburgh]] <small>([[Master of Arts (Scotland)|MA]])</small>
| alma_mater = [[Chuo Kikuu cha Makerere]] <small>([[Diploma of Education|DipEd]])</small> <br> [[University of Edinburgh]] <small>([[Master of Arts (Scotland)|MA]])</small>
| occupation =
| occupation =
| profession = Mwalimu
| profession = Mwalimu
| religion = [[Ukirsto]] ([[Katoliki]])
| religion = [[Ukristo]] ([[Katoliki]])
| signature =
| signature =
| signature_alt =
| signature_alt =

Pitio la 22:13, 2 Mei 2013

Mwalimu Julius Nyerere


Muda wa Utawala
26 April 1964 – 5 November 1985
Waziri Mkuu Rashidi Kawawa (1972–1977)
Edward Sokoine (1977–1980)
Cleopa Msuya (1980–1983)
Edward Sokoine (1983–1984)
Salim Ahmed Salim (1984–85)
Makamu wa Rais Abeid Karume (1964–1972)
Aboud Jumbe (1972–1984)
Ali Hassan Mwinyi (1984–1985)
aliyemfuata Ali Hassan Mwinyi

Rais wa Tanganyika
Muda wa Utawala
9 December 1962 – 25 April 1964
Waziri Mkuu Rashidi Kawawa

Waziri Mkuu wa Tanganyika
Muda wa Utawala
1 May 1961 – 22 January 1962
Monarch Elizabeth II
mtangulizi Ofisi iliundwa
aliyemfuata Rashidi Kawawa

Waziri Kiongozi wa Tanganyika
Muda wa Utawala
2 September 1960 – 1 May 1961
Monarch Elizabeth II

tarehe ya kuzaliwa (1922-04-13)13 Aprili 1922
Butiama, Tanganyika
tarehe ya kufa 14 Oktoba 1999 (umri 77)
London, United Kingdom
mahali pa kuzikiwa Butiama, Tanzania
utaifa Mtanzania
chama CCM
ndoa Maria Nyerere
watoto 7
mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere (DipEd)
University of Edinburgh (MA)
Fani yake Mwalimu
dini Ukristo (Katoliki)
tovuti juliusnyerere.info

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa rais wa kwanza wa Tanzania. Alizaliwa Butiama, mkoani Mara pembezoni mwa Ziwa Nyanza tarehe 13 Aprili 1922. Alifariki dunia 14 Oktoba 1999. Aliiongoza Tanzania toka mwaka 1961 hadi mwaka 1985.

Yeye ni mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea. Kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa ni mwalimu. Kazi hii ndiyo ilimpatia jina ambalo lilimkaa maisha yake yote la "Mwalimu." Mwalimu Nyerere ni kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameacha madaraka kwa hiyari baada ya kutawala kwa muda mrefu. Alipostaafu urais mwaka 1985 alirudi kijijini kwake Butiama ambako aliendesha shughuli za kilimo. Aliendelea kuwa na athari kubwa katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake.

Maisha yake

Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka 1922 ( katika kijiji cha Butiama, wilaya ya Musoma, mkoa wa Mara, Tanzania (wakati ule: Tanganyika). Alikuwa mojawapo kati watoto 26 wa Nyerere Burito, chifu wa kabila la Wazanaki. Alipokuwa mtoto Nyerere alichunga mifugo ya babake; katika umri wa miaka 12 aliingia shule akitembea kilomita 30 hadi Musoma. Baada ya kumaliza shule ya msingi aliendelea kusoma shule ya wamisionari Wakatoliki huko Tabora. Katika umri wa miaka 20 alibatizwa akawa mkristo Mkatoliki hadi mwisho wa maisha yake.

Mapadre wakaona akili yake wakamsaidia kusoma ualimu huko Makerere, Kampala, Uganda kuanzia 1943 - 1945. Makerere akaanzisha tawi la Umoja wa wanafunzi Watanganyika pia amejihusisha na tawi la Tanganyika African Association (TAA). Baada ya kumaliza masomo ya ualimu alirudi Tabora akifundisha shule ya St.Mary´s. Mwaka 1949 alipata skolashipu ya kwenda kusoma kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh huko Uskoti / Uingereza akasoma M.A. ya historia na uchumi(alikuwa mtanzania wa kwanza kusoma katika chuo kikuu cha Uingereza na mtanzania wa pili kupata shahada ya elimu ya juu nje ya Tanzania).

Aliporejea Tanganyika kutoka masomoni, Nyerere alifundisha Historia, Kingereza na Kiswahili katika shule ya St. Francis iliyo karibu na Dar es Salaam. Mwaka 1953 alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African Association (TAA), chama ambacho alikisaidia kukijenga alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere. Mwaka 1954 alikibadilisha chama cha TAA kwenda katika chama cha Tanganyika African National Union (TANU) ambacho kilikuwa cha kisiasa zaidi kuliko TAA. Ndani ya mwaka mmoja chama cha TANU kilikuwa tayari chama cha siasa kinachoongoza Tanganyika.

Uwezo wa mwl. Nyerere uliwashitua uongozi wa kikoloni na kumlazimisha Nyerere kuchagua kati ya siasa na kazi ya ualimu. Nyerere alisikika akisema kuwa alikuwa mwalimu kwa kuchagua na mwanasiasa kwa bahati mbaya. Alijiuzuru ualimu na kuzunguka nchini Tanganyika kuzungumza na watu wa kawaida na machifu ili kuleta muungano katika mapigano ya uhuru. Pia alizungumza kwa niaba ya TANU katika Trusteeship council na Fourth committee ya Umoja wa Mataifa (UN) huko New York. Uwezo wake wa kimaongezi na kuunganisha watu ulimwezesha kufanikisha Tanganyika kupata uhuru bila umwagaji wa damu. Ushirikiano mzuri aliouonyesha aliyekuwa gavana wa wakati huo bwana Richard Turnbull ulisaidia pia kuharakisha upatikanaji wa uhuru. Nyerere aliingia katika bunge la kikoloni mwaka 1958 na kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka 1960. Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wake na tarehe 9/12/1961 Nyerere alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika huru na mwaka mmoja baadae Nyerere alikuwa raisi wa kwanza wa jamhuri ya Tanganyika. Nyerere alikuwa kiungo muhimu katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania baada ya mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 yaliyomtoa madarakani sultani wa Zanzibar Jamshid bin Abdullah.

Julius Nyerere mzee mnamo 1977

05.02.1977 aliongoza chama cha TANU katika tendo la kuungana na chama tawala cha Zanzibar ASP na kuanzisha chama kipya cha CCM (Chama cha Mapinduzi) akiwa mwenyekiti wake.

Nyerere aliendelea kuongoza Taifa hadi 1985 alipomwachia nafasi raisi wa pili Ali Hassan Mwinyi. Aliendelea kuongoza Chama cha CCM hadi 1990 na kuwa na athari kubwa katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake. Inasadikika kuwa Nyerere alishawishi uteuzi wa Benjamini W.Mkapa kama mgombea wa raisi wa mwaka 1995 na ambaye aliteuliwa kuwa raisi kwenye uchaguzi wa mwaka 1995. Nyerere alikaa muda mwingi kwake Butiama akilima shamba lake. Pamoja na haya alianzisha taasisi yenye jina lake; mwaka 1996 alionekana akiwa mpatanishi wa pande mbalimbali wa vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Burundi. Tar. 14.10.1999 aliaga dunia katika hospitali ya St Thomas London baada ya kupambana na kansa ya damu.

Mafanikio na kasoro

Makala hii bado inahitaji maelezo na utathmini zaidi kuhusu kazi ya Mwalimu Nyerere; labda hivi:
Nyerere akichanganya ardhi za Zanzibar na Tanganyika wakati wa muungano 1964

Mafanikio

(kujenga umoja wa Taifa na utamaduni wa Kiafrika pamoja na lugha ya Kiswahili, kushinda ubaguzi wa rangi, kutetea usalama wa taifa katika vitani dhidi Idi Amin)

Kutoa mchango kwa vyama vya ukombozi vya nchi za kusini ya Afrika kama; Zimbabwe {ZANU), Afrika Kusini (ANC na PAC), Namibia (SWAPO), Angola (MPLA) na Msumbiji (Frelimo)

Kutofanikiwa

Siasa zake za ujamaa zilishindwa baada ya mwaka 1976.

Baada ya kuona kuwa uchumi wa Tanzania hautaweza kusimama kwa siasa za kijamaa na kutoweza kuvumilia kuendesha nchi kwa siasa ambazo yeye hakuwa muumini, Nyerere kwa maamuzi yake mwenyewe aliamua kustaafu nafasi ya uraisi baada ya uchaguzi wa mwaka 1985 na kumwachia usukani kwa Ali Hassan Mwinyi aliyetawala kwa siasa za uchumi wa soko huria.

Katika hali ya kukubali ukweli, Nyerere alitamka katika tafrija ya kumwaga juu ya siasa yake kiuchumi “Nimefeli. Tukubali hivyo.”

Ukosoaji dhidi yake

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Mwl.Nyerere analaumiwa kwa siasa zake za kiujamaa kuwa zilichelewesha maendeleo ya kiuchumi wa Tanzania.

Pia kuna makundi ya waislamu wanaomtuhumu kwa kuendesha kwa siri vita dhidi ya uislamu na upendeleo wa elimu na madaraka kwa wakristo,japo wasomi wengi kwa kipindi cha utawala wake walikuwa wakristo.

Nyerere akicheza bao kwake Butiama akitazamwa na mfuasi wake katika urais Ali Hassan Mwini, mke wake Maria na kakaye chifu Burito

Sifa zake

Bado anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu.Pia ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika.

Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi ya 24.

Kaburi la Nyerere kijijini Butiama

Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima wa kawaida kijijini kwake Butiama. Alipatwa na kansa ya damu (leukemia) na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa katika mji wa London tarehe 14 Oktoba 1999. Alizikwa mahali pa kuzaliwa kwake, kijiji cha Butiama.

Machapisho ya mwl.Julius K. Nyerere.

Freedom and Socialism.Mkusanyiko wa maandiko na hotuba, 1965-1967 (1968)

Freedom & Development, Uhuru Na Maendeleo (1974)

Ujamaa - Essays on Socialism' (1977)

Crusade for Liberation (1979)

Julius Kaisari.Tafsiri ya mchezo wa William Shakespeare unaoitwa Julius Caesar

Viungo vya nje