Mkondo wa Benguela : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Addbot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 31 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q59676 (translate me)
Legobot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 1 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q59676 (translate me)
 
Mstari 12: Mstari 12:
[[Jamii:Mikondo ya Bahari]]
[[Jamii:Mikondo ya Bahari]]
[[Jamii:Jiografia ya Namibia]]
[[Jamii:Jiografia ya Namibia]]

[[eu:Benguelako itsaslasterra]]

Toleo la sasa la 11:15, 11 Machi 2013

Mkondo wa Benguela kati ya mikondo ya Atlantiki ya Kusini
mikondo baridi kwa rangi ya buluu - mikondo ya vuguvugu kwa rangi nyekundu

Mkondo wa Benguela ni mkondo wa bahari katika Atlantiki ya Kusini unaotoka katika bahari baridi karibu na Antaktika na kuelekea kaskazini ukipita kwenye pwani la magharibi la Afrika. Mkondo una upana wa 200-3000 km.

Mkondo husukuma maji baridi kwenye pwani la Afrika Kusini, Namibia na Angola. Maji yake huwa vuguvugu kiasi jinsi inavyofika kaskazini katika halijoto ya juu zaidi. Karibu na ikweta unabadilika mwelekeo wake na kuingia katika mkondo wa kusini ya ikweta. Sehemu ya maji yake inaingia katika bahari ya Karibi na kulisha mkondo wa ghuba.

Kusini ya rasi ya Afrika mkondo wa Benguela unakutana na maji ya vuguvugu ya mkondo wa Agulhas kutoka Bahari Hindi.

Athira kwa hali ya hewa Namibia[hariri | hariri chanzo]

Ukipita kwenye pwani la Namibia husababisha hali ya hewa kavu sana. Baridi ya mkondo wa Benguela hupoza upepo kutoka kusini-magharibi na kuusababisha kunyesha unyevu wake kama mvua baharini hivyo kuzuia mvua barani. Jangwa la Namib ni tokeo la mazingira haya. Halijoto ya maji kwenye mwambao wa Namibia huwa ni kwenye 15 °C na ukungu hutokea mara kwa mara mwambaoni.