Karl Marx : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.7.2+) (Roboti: Imeongeza ba:Карл Маркс
Addbot (majadiliano | michango)
d Bot: Migrating 146 interwiki links, now provided by Wikidata on d:q9061 (translate me)
Mstari 100: Mstari 100:
{{Link FA|la}}
{{Link FA|la}}


[[af:Karl Marx]]
[[am:ካርል ማርክስ]]
[[an:Karl Marx]]
[[ar:كارل ماركس]]
[[arz:كارل ماركس]]
[[as:কাৰ্ল মাৰ্ক্স]]
[[ast:Karl Marx]]
[[ay:Karl Marx]]
[[az:Karl Marks]]
[[ba:Карл Маркс]]
[[bat-smg:Karls Marksos]]
[[bcl:Karl Marx]]
[[be:Карл Маркс]]
[[be-x-old:Карл Маркс]]
[[bg:Карл Маркс]]
[[bn:কার্ল মার্ক্স]]
[[bo:ཁཱར་ལ་མར་ཁེ་སི།]]
[[bpy:কার্ল মার্ক্স্]]
[[br:Karl Marx]]
[[bs:Karl Marx]]
[[ca:Karl Marx]]
[[ckb:کارڵ مارکس]]
[[co:Karl Marx]]
[[cs:Karl Marx]]
[[cv:Карл Маркс]]
[[cy:Karl Marx]]
[[da:Karl Marx]]
[[de:Karl Marx]]
[[diq:Karl Marx]]
[[dsb:Karl Marx]]
[[el:Καρλ Μαρξ]]
[[en:Karl Marx]]
[[eo:Karl Marx]]
[[es:Karl Marx]]
[[et:Karl Marx]]
[[eu:Karl Marx]]
[[ext:Karl Marx]]
[[fa:کارل مارکس]]
[[fi:Karl Marx]]
[[fiu-vro:Marxi Karl]]
[[fr:Karl Marx]]
[[fy:Karl Marx]]
[[ga:Karl Marx]]
[[gan:馬克思]]
[[gd:Karl Marx]]
[[gl:Karl Marx]]
[[glk:کارل مارکس]]
[[he:קרל מרקס]]
[[hi:कार्ल मार्क्स]]
[[hif:Karl Marx]]
[[hr:Karl Marx]]
[[hsb:Karl Marx]]
[[hu:Karl Marx]]
[[hy:Կառլ Մարքս]]
[[hy:Կառլ Մարքս]]
[[ia:Karl Marx]]
[[id:Karl Marx]]
[[ilo:Karl Marx]]
[[io:Karl Marx]]
[[is:Karl Marx]]
[[it:Karl Marx]]
[[ja:カール・マルクス]]
[[jbo:karl. marks]]
[[jv:Karl Marx]]
[[ka:კარლ მარქსი]]
[[kaa:Karl Marx]]
[[kab:Karl Marx]]
[[kk:Карл Маркс Генрих]]
[[kn:ಕಾರ್ಲ್ ಮಾರ್ಕ್ಸ್]]
[[ko:카를 마르크스]]
[[ku:Karl Marx]]
[[ky:Маркс, Карл]]
[[la:Carolus Marx]]
[[lad:Karl Marx]]
[[lb:Karl Marx]]
[[lez:Карл Маркс]]
[[li:Karl Marx]]
[[lmo:Karl Marx]]
[[lt:Karl Marx]]
[[lv:Kārlis Markss]]
[[mk:Карл Маркс]]
[[ml:കാൾ മാർക്സ്]]
[[mn:Карл Маркс]]
[[mr:कार्ल मार्क्स]]
[[ms:Karl Marx]]
[[mt:Karl Marx]]
[[mwl:Karl Marx]]
[[my:ကားလ်မာ့ခ်]]
[[mzn:کارل مارکس]]
[[nah:Karl Marx]]
[[nds:Karl Marx]]
[[nds-nl:Karl Marx]]
[[ne:कार्ल मार्क्स]]
[[nl:Karl Marx]]
[[nn:Karl Marx]]
[[no:Karl Marx]]
[[nov:Karl Marx]]
[[oc:Karl Marx]]
[[pa:ਕਾਰਲ ਮਾਰਕਸ]]
[[pl:Karol Marks]]
[[pms:Karl Marx]]
[[pnb:کارل مارکس]]
[[pnt:Καρλ Μαρξ]]
[[ps:کارل مارکس]]
[[pt:Karl Marx]]
[[qu:Karl Marx]]
[[rm:Karl Marx]]
[[ro:Karl Marx]]
[[ru:Маркс, Карл]]
[[rue:Карл Маркс]]
[[sa:कार्ल मार्क्स]]
[[sah:Карл Маркс]]
[[sc:Karl Marx]]
[[scn:Karl Marx]]
[[sco:Karl Marx]]
[[sh:Karl Marx]]
[[si:කාල් මාක්ස්]]
[[simple:Karl Marx]]
[[sk:Karl Marx]]
[[sl:Karl Marx]]
[[so:Karl Marx]]
[[sq:Karl Marx]]
[[sr:Карл Маркс]]
[[st:Karl Marx]]
[[su:Karl Marx]]
[[sv:Karl Marx]]
[[ta:கார்ல் மார்க்சு]]
[[te:కార్ల్ మార్క్స్]]
[[tg:Карл Маркс]]
[[th:คาร์ล มาร์กซ์]]
[[tl:Karl Marx]]
[[tr:Karl Marx]]
[[tt:Карл Маркс]]
[[ug:كارل ماركىس]]
[[uk:Карл Маркс]]
[[ur:کارل مارکس]]
[[uz:Karl Marx]]
[[vi:Karl Marx]]
[[wa:Karl Marx]]
[[war:Karl Marx]]
[[xmf:კარლ მარქსი]]
[[yi:קארל מארקס]]
[[yo:Karl Marx]]
[[za:Karl Marx]]
[[zea:Karl Marx]]
[[zh:卡尔·马克思]]
[[zh-min-nan:Karl Marx]]
[[zh-yue:馬克思]]

Pitio la 18:43, 9 Machi 2013

Karl Marx

Karl Marx (1818 - 1883) alikuwa mwanafalsafa kutoka nchini Ujerumani ambaye pamoja na Friedrich Engels alianzisha ukomunisti.

Maisha yake

Alizaliwa mjini Trier tarehe 5 Mei 1818.

Kati ya 1835 na 1841 alisoma sheria, historia na falsafa.

Tangu 1842 alikuwa mwandishi mkuu wa gazeti la Rheinische Zeitung mjini Köln. Alisimama upande wa wafuasi wa demokrasia dhidi ya utawala wa watemi na wafalme katika Ujerumani.

Kutokana na upinzani huo serikali ya Prussia ilimkataza asiandike tena kwenye magazeti, hivyo alihamia Ufaransa. Alipokaa mjini Paris alianza kuandika juu ya ujamaa kama ukamilisho wa demokrasia.

Baada ya kuhamia Brussels katika Ubelgiji alitunga pamoja na Engels kijitabu cha Manifesto ya Chama cha Kikomunisti (Ilani ya kikomunisti) alimotangaza imani yake ya kwamba "historia ya jamii zote ni historia ya mapambano ya matabaka". Alichora picha ya historia ambako jamii ya kikabaila imezaa ngazi mpya ya ubepari; hapo alitabiri kwamba ubepari utazaa tena mbegu wa uharibifu wake na utafuatwa na ujamaa au ukomunisti. Ukomunisti utakuwa na jamii bila matabaka na bila utawala. Aliona ya kwamba wafanyakazi kama tabaka linalozalisha utajiri wanapaswa kuchukua utawala mikononi mwao kwa njia ya mapinduzi akawaalika, "Wafanyakazi wa nchi zote muungane!".

Baadaye Marx alipaswa kukimbia Ulaya bara akapata kimbilio Uingereza alipoishi London hadi kifo chake, akitumia muda mwingi kwenye maktaba ya Britania. Alikuwa na vipindi vya umaskini mkali lakini alipata tena msaada kutoka kwa rafiki yake Engels. Kwa miaka kadhaa alikuwa mwanahabari wa gazeti la Marekani "New York Tribune".

Huko London aliandika kitabu chake kikuu "Das Kapital" (yaani "Rasilmali").

Aliaga dunia tarehe 14 Machi 1883 akazikwa kwenye makaburi ya Highgate Cemetery.

Falsafa yake

Kwa Marx kazi ya falsafa haikuwa kueleza dunia ilivyo bali kuibadilisha. Alifundisha ya kwamba mawazo, fikra na imani zote zinatokana na hali ya uchumi na teknolojia katika jamii.

Mwenyewe aliathiriwa sana na Georg Wilhelm Friedrich Hegel na kutoka kwake alipokea hoja ya kuwa historia linafuata kanuni zake likielekezwa kwenye lengo maalumu. Tofauti na Hegel aliona historia haisukumwi na "roho ya ulimwengu" bali na nguvu za uchumi wa jamii na namna ya kujipatia riziki za maisha.

Kutokana na msingi huu Marx alikataa dini na imani ya Mungu. Kwake dini ni itikadi ya jamii ya uwongo na pamoja na sahihisho la jamii alitarajia ya kwamba dini itapotea.

Matokeo yake

Baada ya kifo chake Engels aliendelea kutoa maandiko yake kama vitabu.

Marx alikuwa na athira kubwa kati ya vyama vya wafanyakazi vya Ulaya vyenye mwelekeo wa kisoshalisti.

Baadaye kundi kali kati ya wasoshalisti Warusi chini ya Lenin iliendelea kupanua mafundisho ya Marx kwa "Umarx-Ulenin" iliyokuwa itikadi rasmi ya vyama vya kikomunisti.

Marx aliheshimiwa kama nabii katika nchi zilizotawaliwa na Wakomunisti, kuanzia Urusi hadi kuenea kwa thuluti moja ya watu wote duniani.

Hasa kuanzia mwaka 1989 athari yake imepungua.

Viungo vya Nje

Maandiko yake

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Maisha yake

Makala na kamusi

Kigezo:Link FA