Ali ibn Abu Talib : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d Roboti: Imeongeza tl:Ali ibn Abi Talib
d r2.7.2+) (Roboti: Imeongeza ba:Али (Ғәли) Әбү Талип
Mstari 41: Mstari 41:
[[arz:على بن ابى طالب]]
[[arz:على بن ابى طالب]]
[[az:Əli bin Əbu Talib]]
[[az:Əli bin Əbu Talib]]
[[ba:Али (Ғәли) Әбү Талип]]
[[be:Алі ібн Абу Таліб]]
[[be:Алі ібн Абу Таліб]]
[[be-x-old:Алі]]
[[be-x-old:Алі]]

Pitio la 18:16, 23 Februari 2013

Picha ya Kiajemi ya kisasa ya Ali

Ali Ibn Abu Talib (Kar.: علي ابن أبي طالب * mnamo 600 BK Makka - + Januari 661 Kufah / Irak) alikuwa mkwe wa mtume Muhammad, khalifa wa nne wa Uislamu na imamu wa Shia wa kwanza. Alikuwa pia baba wa wajukuu wa pekee wa mtume.

Aheshimiwa na Washia kama mfuasi wa kweli wa pekee wa mtume.

Binamu na mkwe wa Mtume

Ali alikuwa binamu wa Mohammed na kati ya wafuasi wa kwanza wa mtume. Alimwoa Fatimah binti wa mtume akazaa naye watoto watano: * Hasan ibn Ali (imamu wa pili wa Shia)

Swali la khalifa

Baada ya kifo cha Muhammad mwaka 632 swali la kiongozi mpya wa umma wa Waislamu likaleta fitina kati ya wafuasi wa Ali na wengine iliyosababisha hadi leo mgawanyo kati ya Wasunni na Washia.

Mkutano wa viongozi Waislamu ulimchagua Abu Bakr kuwa khalifa wa kwanza badala ya Ali aliyedai ya kwamba aliteuliwa na mtume mwenyewe kuwa kiongozi baada yake. Hata baada ya kifo cha Abu Bakr wakateuliwa mara mbili makhalifa wengine yaani Umar ibn al-Khattab kama khalifa wa pili halafu Uthman ibn Affan kama khalifa wa tatu.

Msikiti mahali pa kaburi la Ali mjini Najaf (Irak)

Khalifa wa nne

Ni baada ya kuuawa kwa Uthman tu ya kwamba Ali alichaguliwa khalifa wa nne. Alihamia Kufa nchini Irak penye kituo kikubwa cha jeshi la Uislamu.

Tangu mwanzo aliona upinzani wa vikundi mbalimbali si Waislamu wote waliomkubali:

  • wengine walimshatki ya kwamba alishiriki katika mauaji ya Uthman
  • Aisha mjane wa mtume alikusanya jeshi kutoka Makka dhidi yake akamshambulia Ali katika mapigano ya ngamia lakini alishindwa naye
  • Muawiya jemadari Mwislamu wa Dameski na ndugu wa Uthman aliyeuawa aliasi dhidi ya Ali. Mwaka 657 majeshi yao yalikutana Siffin na Ali alipaswa kukubali amani bila kuweza kumwondoa Muawwiyya.
  • Tendo la kupatana na Muawiyya likasababisha Wakharijiya kuasi dhidi ya Ali
Msikiti mjini Mazar-e-Sharif (Afghanistan) ambako Washia wa Afghanistan huamini iko kaburi la Ali

Kifo na kutokea kwa Shia

Tar. 22 Januari 661 Ali aliuawa na Mkharijiya huko Kufa. Watoto wake Hasan na Husain walishindwa kumfuata kwa sababu Muawiya alichukua utawala akiwa khalifa wa tano.

Swali hili la uongozi ulisababisha fitina na mgawanyo kati ya Waislamu. "Shiat Ali" (chama cha Ali) ilikuwa sasa mwendo wa pekee ndani ya Uislamu uliodai ya kwamba uongozi wapaswa kuwa mkononi wa familia ya mtume hivyo wa watoto na wajukuu wa Ali na Fatimah.

Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA