Katerina wa Siena : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d Roboti: Imeongeza eu:Katalina Sienakoa
d r2.7.2) (Roboti: Imeongeza simple:Catherine of Siena
Mstari 165: Mstari 165:
[[sc:Caderina]]
[[sc:Caderina]]
[[scn:Santa Catarina di Siena]]
[[scn:Santa Catarina di Siena]]
[[simple:Catherine of Siena]]
[[sl:Sveta Katarina Sienska]]
[[sl:Sveta Katarina Sienska]]
[[sq:Shën Katrina e Sienës]]
[[sq:Shën Katrina e Sienës]]

Pitio la 08:54, 6 Februari 2013

Madonda matakatifu ya Katerina wa Siena yalivyochorwa na Domenico Beccafumi, mwaka 1515 hivi

Katerina Benincasa wa Siena (25 Machi 1347 - 29 Aprili 1380) alikuwa mfuasi wa Dominiko Guzman, mwenye vipaji na karama za pekee.

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu bikira na mwalimu wa Kanisa.

Pia ni msimamizi wa Italia (kwa uamuzi wa Papa Pius XII mwaka 1939) na wa Ulaya (kwa uamuzi wa Papa Yohane Paulo II mwaka 1999).

Maisha

Utoto

Katerina alizaliwa Siena (Italia) kama mtoto wa 24 kati ya 25 wa Jacopo Benincasa, na Lapa Piagenti (au Piacenti). Pacha wake Giovanna (kitindamimba) aliishi miezi tu.

Mwaka uliofuata (1348) Siena na Ulaya kwa jumla zilipatwa na tauni iliyopunguza sana idadi ya watu.

Alisimulia kwamba alipokuwa na miaka sita alianza kupata njozi na akiwa na miaka saba aliweka nadhiri ya ubikira akianza safari ya toba yenye saumu na malipizi mengine.

Kwenye miaka 12 wazazi, wasiojua nadiri yake, walianza kufikiria ndoa yake. Katerina aliitikia hata kwa kunyoa kipara na kujifungia nyumbani. Ili kumshurutisha wazazi walimuagiza kazi nzito nyingi, lakini bure. Siku moja baba alimkuta akisali ana njiwa akielea kichwani pake. Hapo alikubali kumuacha huru ajichagulie maisha.

Kujiunga na Wadominiko

Alipokuwa na miaka 16 alijiunga na Utawa wa Tatu wa Mt. Dominiko bila ya kuhama nyumbani.

Alijaribu kusoma vitabu vitakatifu bila ya kufundishwa, mpaka hatimaye alijaliwa kipawa cha kusoma. Baadaye tena akajaliwa kuandika, lakini maandishi yake mengi aliyaandikisha tu.

Alisimulia pia kwamba kabla ya Kwaresima ya mwaka 1367 alitokewa na Yesu pamoja na Bikira Maria na watakatifu wengine ili kumuoa kiimani, akimvika pete yenye rubi aliyoweza kuiona yeye tu.

Uhusiano na viongozi wa Kanisa na wa siasa

Katerina hakuogopa watu wakubwa bali aliwaelekea uso kwa uso bila ya unyonge. Kwenye mwaka 1372 hivi alimueleza balozi wa Papa huko Italia, Pietro d'Estraing, haja ya kurekebisha maadili ya makleri, ya kumrudisha Papa toka Avignone (watangulizi wake na yeye walipokaa tangu mwaka 1309) hadi Roma na ya kuendesha vita vya msalaba dhidi ya wasioamini.

Viongozi wa juu wa Kanisa, wakichukizwa na ushujaa wa mwanamke huyo asiye na elimu, walimuita mwaka 1374 huko Firenze mbele ya mkutano mkuu wa Wadominiko. Shirika lao lilitambua usahihi wa imani yake na kumkabidhi kwa uongozi wa kiroho wa Raimondo wa Capua (1330-1399) ambaye baadaye aliandika maisha yake.

Inasemekana kuwa tarehe 1 Aprili 1375 huko Pisa alijaliwa madonda matakatifu yasiyoonekana hadi kifo chake.

Baada ya majaribio mengi, hatimaye alifaulu katika juhudi kuu ya maisha yake: tarehe 17 Januari 1377 Papa alihamia Roma.

Mwanzoni mwa 1378 aliagizwa kupatanisha Ukulu mtakatifu na Firenze.

Lakini tarehe 20 Septemba wa mwaka huohuo, huko Fondi, lilianza Farakano la magharibi litakalodumu miaka 40 kwa madhara makubwa.

Alifariki akiwa na miaka 33 tu, baada ya kushindwa kula na kunywa muda mrefu kutokana na njozi ya Yesu Kristo aliyemjalia kufyonza damu ubavuni mwake.

Utukufu

Katerina da Siena alitangazwa na Papa Pius II kuwa mtakatifu mwaka 1461. Papa Paulo VI alimtangaza mwalimu wa Kanisa tarehe 4 Oktoba 1970.

Sala zake

Mungu wa milele, Utatu wa milele, umefanya damu ya Kristo iwe azizi kabisa kwa kushiriki umungu wako.

Wewe ni fumbo la kina kuliko bahari; kadiri ninavyotafuta naona; na kadiri ninavyoona nakutafuta.

Siwezi kamwe kushiba; ninachopokea kitanifanya daima nitamani zaidi.

Unapojaza roho yangu nazidi kuonea njaa na shauku mwanga wako.

Hasa natamani kukuona wewe, mwanga halisi, jinsi ulivyo.

Ndiwe muumba wangu, Utatu wa milele, nami ni kiumbe chako.

Umenifanya kiumbe kipya katika damu ya Mwanao, nami najua unavutwa na uzuri wa kiumbe chako kutokana na upendo.


Bwana wangu, elekeza jicho la huruma yako juu ya taifa lako na juu ya mwili wa fumbo wa Kanisa takatifu.

Wewe utatukuzwa zaidi sana kwa kusamehe na kuwaangazia akili wengi, kuliko kwa kupokea heshima toka kwa kiumbe mmoja duni, kama nilivyo mimi, ambaye nilikukosea sana na kuwa sababu na chombo cha maovu mengi.

Ingenitokea nini kama ningeona mimi ni hai, na watu wako wamekufa?

Ingekuwaje kama ningeliona gizani, kutokana na dhambi zangu na za viumbe wengine, Kanisa lako, Bibiarusi wako mpenzi, lililozaliwa liwe mwanga?

Basi, nakuomba huruma kwa taifa lako kwa ajili ya ya upendo usioumbwa uliokusukuma wewe umuumbe mtu kwa sura na mfano wako.

Sababu gani ilikufanya umweke mtu katika heshima kubwa hivyo?

Bila ya shaka ni upendo ule usiothaminika ambao ulimuangalia kiumbe chako ndani mwako ukachanganyikiwa naye.

Lakini baadaye kwa dhambi aliyoitenda akapoteza ukuu huo uliomuinulia.

Ukisukumwa na moto huohuo ambao ulituumba, ulipenda kuwatolea binadamu njia ya kupatanishwa nawe.

Ndiyo sababu umetupatia Neno, Mwanao pekee.

Amekuwa mshenga kati yako na sisi, amekuwa haki yetu aliyeadhibu ndani mwake maovu yetu.

Alitii agizo ambalo wewe, Baba wa milele, ulimpa ulipomvika utu wetu.

Lo, kilindi cha upendo! Moyo upi hautajaa mhemko kwa kuona ukuu huo kushukia unyonge mkubwa kama huu, yaani ubinadamu wetu?

Sisi ni mfano wako, nawe mfano wetu kutokana na muungano uliouanzisha kati yako na binadamu, ukifunika umungu wa milele kwa wingu maskini la utu ulioharibika wa Adamu.

Kwa sababu gani? Bila ya shaka kwa upendo.

Kwa upendo huo usiosemeka nakuomba na kukuhimiza uwawie huruma viumbe wako.

Maandishi

  • Maongezi ya Maongozi ya Mungu yaani Kitabu cha mafundisho ya Mungu
  • Barua 381
  • Sala [26/27]

Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA