Kitabu cha Malaki : Tofauti kati ya masahihisho
d r2.6.8) (Robot: Modifying yo:Ìwé Malaki to yo:Ìwé Málákì |
Xqbot (majadiliano | michango) d r2.7.3) (Robot: Modifying da:Malakias’ Bog to da:Malakias' Bog |
||
Mstari 49: | Mstari 49: | ||
[[ceb:Basahon ni Malaquías]] |
[[ceb:Basahon ni Malaquías]] |
||
[[cs:Kniha Malachiáš]] |
[[cs:Kniha Malachiáš]] |
||
[[da: |
[[da:Malakias' Bog]] |
||
[[en:Book of Malachi]] |
[[en:Book of Malachi]] |
||
[[eo:Libro de Malaĥi]] |
[[eo:Libro de Malaĥi]] |
Pitio la 15:42, 11 Desemba 2012
Kitabu cha Malaki ni cha mwisho kati ya vitabu 12 vya Manabii wadogo ambavyo, pamoja na vingine vingi, vinaunda Tanakh, yaani Biblia ya Kiebrania. Hivyo ni pia sehemu ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo, na kwa kuwa humo vitabu vya manabii vinapangwa baada ya vitabu vya hekima, kitabu cha Malaki ni cha mwisho kabla ya vitabu vya Agano Jipya.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Mwandishi na jina
Kwa kuwa jina la nabii aliye asili ya kitabu hiki halijulikani, limetumika lile la neno lake muhimu zaidi, "Malaki", lenye maana ya "Mjumbe wangu" (kwa Kiebrania מלאכי).
Muda
Yaliyomo yanawezesha kukisia kiliandikwa lini, yaani baada ya Hekalu la Yerusalemu kuwekwa wakfu (515 K.K.), na kabla ya katazo la ndoa za mseto kati ya Wayahudi na mataifa mengine lililotolewa na Nehemia (445 K.K.); sanasana ni karibu na mwaka huo.
Muhtasari
Kitabu kinaundwa na sehemu sita za namna ileile: Mungu (au nabii wake) anatoa kauli ambayo inajadiliwa na waamini na makuhani wao, halafu inafafanuliwa katika hotuba inayochanganya vitisho na ahadi za wokovu.
Mada kuu ni mbili: makosa ya makuhani na waamini wengine katika ibada, halafu makwazo yanayosababishwa na ndoa za mseto.
Nabii anatabiri siku ya YHWH atakayetakasa makuhani, ataangamiza waovu na kuwapa ushindi waadilifu.
Mistari ya mwisho, ikitabiri ujio wa pili wa nabii Eliya, ilivutia sana tumaini la Wayahudi; ndiyo sababu ilijadiliwa sana kuhusiana na Yohane Mbatizaji na Yesu Kristo, kama inavyoonekana katika sehemu mbalimbali za Injili.
Marejeo
- New American Bible - http://www.usccb.org/nab/bible/malachi/malachi1.htm
- 21st Century KJV - http://www.biblegateway.com/passage/?search=Malachi+1&version=KJ21
- NIRV - http://www.biblegateway.com/passage/?search=Malachi+1&version=NIRV
- Malachi at Chabad.org - http://www.chabad.org/library/bible_cdo/aid/16219
- Easton's Bible Dictionary, 1897.
- Hill, Andrew E. Malachi: A New Translation with Introduction and Commentary. The Anchor Bible Volume 25D. Toronto: Doubleday, 1998.
- LaSor, William Sanford et al. Old Testament Survey: the Message, Form, and Background of the Old Testament. Grand Rapids: William B. Eerdmans, 1996.
- Mason, Rex. The Books of Haggai, Zechariah and Malachi. The Cambridge Bible Commentary on the New English Bible. New York, Cambridge University Press, 1977.
- Singer, Isidore & Adolf Guttmacher. "Book of Malachi." JewishEncyclopedia.com. 2002.
Viungo vya Nje
- Kitabu cha Malaki katika tafsiri ya Kiswahili (Union Version)
- Van Hoonacker, A. "Malachias (Malachi)." Catholic Encyclopedia. Transcribed by Thomas J. Bress. 2003.
- The Oracle of Malachi - A verse-by-verse journey through Malachi, connecting 2,500 years ago with today.
Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki
Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.