Kitabu cha Zekaria : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d Roboti: Imeongeza vep:Zaharian kirj
d r2.6.8) (Robot: Modifying yo:Ìwé Sekariah to yo:Ìwé Sẹkaríàh
Mstari 86: Mstari 86:
[[vep:Zaharian kirj]]
[[vep:Zaharian kirj]]
[[yi:זכריה הנביא]]
[[yi:זכריה הנביא]]
[[yo:Ìwé Sekariah]]
[[yo:Ìwé Sẹkaríàh]]
[[zh:撒迦利亞書]]
[[zh:撒迦利亞書]]

Pitio la 09:48, 9 Desemba 2012

Kitabu cha Zekaria ni kimojawapo kati ya vitabu 12 vya Manabii wadogo ambavyo, pamoja na vingine vingi, vinaunda Tanakh, yaani Biblia ya Kiebrania. Hivyo ni pia sehemu ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mwandishi na muda

Kazi ya nabii huyo kati ya mwaka 520 na 518 KK, wakati uleule alipotabiri nabii Hagai, ni mwanzo wa kipindi cha mwisho cha unabii katika Israeli kabla ya ujio wa Yohane Mbatizaji na Yesu Kristo.

Mazingira

Kabla ya uhamisho wa Babeli, ujumbe wa manabii ulitishia mara nyingi adhabu ya Mungu kwa uasi wa taifa lake.

Wakati wa uhamisho ujumbe ulikuwa wa faraja zaidi.

Ule wa Hagai na Zekaria ulilenga ustawi wa Wayahudi ambao walikuwa wamerudi Yerusalemu mwaka 538 K.K. ili kujenga upya hekalu, lakini walichelewa kutekeleza azma yao, kutokana na upinzani na mahangaiko ya kujipatia riziki katika mazingira magumu.

Mbaya zaidi, walikaribia kukata tamaa. Kwa changamoto ya manabii wao, gavana Zerubabeli na kuhani mkuu Yoshua waliongoza wananchi kukazania ujenzi huo na kuukamilisha mwaka 515.

Muhtasari

Kitabu kina sehemu mbili tofauti sana, yaani sura 1-8 halafu 9-14.

Sura nane za kwanza zinaleta njozi kadhaa kuhusu mwanzo mpya wa Wayahudi mjini Yerusalemu.

Tofauti na Hagai, mwandishi wa kitabu hiki hakuishia upande wa ujenzi, bali alisisitiza pia utakaso wa waamini na ibada zao.

Sura nyingine sita zinatokana na mazingira tofauti (ya karne ya 4 K.K.) na kuleta njozi juu ya ujio wa Masiya na siku za mwisho.

Sura hizo zina mtindo wa kiapokaliptiko na wataalamu wengi wanasema ni kazi ya nabii mwingine wanayemuita Zekaria wa pili.

Marejeo

  • The Student Bible, NIV. Michigan: Zondervan Publishing House, 1992.
  • D. Guthrie, (ed.) New Bible Commentary. New York: Eerdmans Publishing Company, 1970.
  • Stephen G. Dempster, Dominion And Dynasty: A Theology Of The Hebrew Bible. Illinois: Intervarsity Press, 2003. ISBN 978-0-8308-2615-5
  • Carroll Stuhlmueller, Haggai and Zechariah: Rebuilding With Hope. Edinburgh: The Handsel Press Ltd., 1988. ISBN 978-0-905312-75-0.

Viungo vya Nje

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.