Kitabu cha Ruthu : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.7.3) (Roboti: Imeongeza vep:Rufin kirj
d r2.6.8) (Robot: Modifying yo:Ìwé Rutu to yo:Ìwé Rútù
Mstari 85: Mstari 85:
[[vi:Sách Rút]]
[[vi:Sách Rút]]
[[yi:מגילת רות]]
[[yi:מגילת רות]]
[[yo:Ìwé Rutu]]
[[yo:Ìwé Rútù]]
[[zea:Ruth (Biebelboek)]]
[[zea:Ruth (Biebelboek)]]
[[zh:路得記]]
[[zh:路得記]]

Pitio la 02:36, 7 Desemba 2012

Katika fujo ya miaka ya Waamuzi (Kitabu cha Waamuzi), habari ya kitabu hiki kifupi inatujenga: inahusu Ruthu, mwanamke Mpagani aliyeolewa na Mwisraeli huko ng’ambo ya mto Yordani.

Baada ya kufiwa mume wake akafuatana na mama mkwe hadi Betlehemu ili aolewe na ndugu wa marehemu na kumzalia mtoto kadiri ya sheria.

Huyo mtoto akawa babu wa mfalme Daudi.

Hivyo kwa uaminifu wake mwanamke huyo pia akatajwa katika Injili kama bibi wa Yesu (Math 1:5-6).

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Mazingira

Habari kuu ya kitabu cha Ruthu ilitokea wakati wa Waamuzi, lakini inafurahisha mojo, ikilinganishwa na hali mbaya ya kidini na kimaadili iliyoandikwa katika kitabu cha Waamuzi. Habari yenyewe inaonyesha kwamba imani kamili kwa Mungu na uangalifu na upendo kwa watu wengine wakati ule pia ulikuwepo katika Israeli. Katika taifa zima walikuwepo watu wengine waliojitahidi kuishi maisha ya unyenyekevu na haki mbele ya Mungu wa kweli. Habari hiyo pia inaonyesha kwamba Mungu aliwaangalia watu kama hao kwa neema yake kubwa, akiyaongoza mambo yao ya kila siku na kuwafanikisha. Wema huo pia ulikuwa baraka kwa taifa zima.

Yaliyomo

1:1-22 Miaka kumi ya taabu katika nchi ya Moabu 2:1-4:22 Mwanzo wa maisha mapya katika Israeli

Viungo vya nje

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.