Zeruzeru : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.7.2+) (Roboti: Imebadilisha: hi:रंगहीनता
d r2.7.2) (roboti Nyongeza: jv:Bulé
Mstari 70: Mstari 70:
[[it:Albinismo]]
[[it:Albinismo]]
[[ja:アルビノ]]
[[ja:アルビノ]]
[[jv:Bulé]]
[[kk:Альбинизм]]
[[kk:Альбинизм]]
[[ko:백색증]]
[[ko:백색증]]

Pitio la 08:49, 6 Septemba 2012

Mvulana albino

Albino (au Zeruzeru) ni ulemavu wa ngozi azaliwao nao mtu, haya ni maelezo mafupi yanayoweza kueleweka kwa mtu wa kawaida. Hali hiyo ya albino huweza kurithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine, huweza kupotea na pia hali hiyo yaweza kubaki katika ukoo au familia fulani na kuwa na mlolongo wa kuzaliwa kwa albino katika familia husika.

Albino ni binadamu mwenye akili timamu, viungo timilifu na mwenye uwezo wa kuzalisha kama mtu mwingine yeyote hapa duniani. Kwa hali ya kawaida, rangi ya mtu kuwa nyeupe sana au nyeusi sana haizuii ubora au kushusha hadhi ya mtu huyo ingawa hali hiyo yaweza kuwa kikwazo tu katika mazingira machache nay a nadra sana. Kwa mfano, Albino akifanaya kazi kwenye jua kali ni rahisi ngozi yake kupata vidonda nah ii hutkana na ukosefu wa vimelea hivyo ambavyo huzuia ngozi isishambuliwe na joto au miali ya jua.

Ni wazi kuwa, watu weupe (Wazungu) hupaka mafuta maalumu wawapo juani na wakati mwingine hujianika juani ili kuongeza virutubisho hivyo mwilini.

Utajiri

Utajiri kwa tafsiri rahisi ni hali ya mtu kuwa na mali nyingi na ambazo humwezesha kuishi kwa namna anavyotaka yeye, hivi karibuni Watanzania walishuhudia ujio wa mmiliki wa timu ya Chelsea ambaye alikodo hoteli nzima pale mjini arusha na kwamba ndege aliokuja nayo ilitosha zaidi ya abiria mia kadhaa, huyo ndiye huitwa tajiri pengine kwa tafsiri rahisi.

Lakini ukweli ni upi kuhusu utajiri wa ma-albino ambao inasadikika wanao bali wao hawajui au pengine hawawezi kuutumia? Kwa kujibu hili inabidi tutazame nini chanzo hasa cha ndugu zangu hawa kuhusishwa na utajiri; historia yake fupi imebebwa na wenzetu hawa waganga wa kienyeji wakiipenyeza dhana hii kwa kupitia wachache wenye uchu wa madaraka, uongozi na au UTAJIRI.

Kwa kuwa waganga hawa wakienyeji na wao niwatafutaji wa maisha kama mtu mwingine yoyote yule, kwa kujua au kutokujua wakaanzisha dhana hii ya kuwa wanao uwezo wa kubadilsha viungo vya albino na kumletea mtu utajiri kwa kupitia kazi yake; kwa mfano mtangazaji wa Ajzeera , Yvone Ndege alipomhoji mmoja wa wanajamii kutoka kanda ya ziwa alifafanua kuwa vioungo hivyo wanapovitumia katika shughuli zao za uvuvi hupata samaki mara dufu. Ni kwa kiasi gain madai hayo yana ukweli, bado ni kitendawili.

Ninachokiamini ni kuwa kwa kuua albino hawa tunapunguza nguvu kazi na kurudi nyuma kimaendeleo badala ya kwenda mbele kama baadhi yetu wanavyodhani, kama kweli viungo hivi vingekuwa vinaleta utajiri basi albino wao wenyewe wengekuwa matajiri sana.

Takwimu

Mpaka kufikia mwezi wa kumi 2009 idadi ya albino ambao waliuwawa kikatili ilikua imezidi arobaini na kwamba ukiacha ambao walifariki kutokana na kuvuja damu na wengine kuumizwa vibaya, asilimia kubwa pia wamebakia vilema na hivyo kutoweza kuzalisha tena.

Zoezi la Uvunaji viungo hivyo

Nimetumia neno UVUNAJI wa viungo ili kuleta hasa maana ya kile kinachofanywa na wahuni hawa kwani tendo hilo hufanyika kama vile watu hawa ni mashamba na mali za kundi hilo.

Albino huviziwa hasa nyakati za usiku au hata kuvamia nyumba, humkamata albino na pasipo kujali maumivu anayoyapata binadamu huyu, mkono, mguu, kidole, kichwa au sehemu nyingine hukatwa hata kama ni sehemu ya siri, huchukuliwa na mhuni huyu hutoweka na sehemu hizo huku albino akiachwa akivuja damu.

Zoezi hili hufanyika sana vijijini ambako hata huduma za afya Faili:Maumivu ya Albino.jpg.hupatikana mbali kidogom, hivyo kitendo cha kumchukua majeruhi huyu na kumkimbizia zahati au hospitali hakusaidii kitu kwani mauti humkuta njiani au wakati mwingine hapo hapo kwenye eneo la tukio.

Tufanye nini sasa?

Kwangu mimi njia ni rahisi kabisa, ingawa msimamo wangu waweza kuwa tofauti kabisa na wengine lakini haya bado yatabaki kuwa mawazo yangu; moja, wanapokamatwa watu hawa, ni vyema wafikishwe kortini haraka iwezekanavyo kasha ikithibitika kwa namna yoyote ile kuwa mtuhumiwa huyo alijihusisha na ukatili huo, mara moja ahukumiwe kifo na sio kifungo cha maisha, tuige mfano wa Wachina waliobainika kuuza maziwa yenye vimelea vya Melamine ambao walikwishahukumiwa adhabu ya kifo.

Pili, kujenga na kuimarisha mifumo yetu ya ulinzi kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa na kuwa na mfumo mzuri wa mawasiliano kwa viongozi wa ngazi zote, ili kukitokea tatizo iwe rahisi kuwasiliana na ngazi husika.

Tatu, hili ni kubwa zaidi, kuelimisha jamii juu ya nini husababisha mtu kuzaliwa albino, maisha yake yalivyo na kwamba hata sisi kwene familia zetu twaweza kupata ma-albino siku moja. Ni vyema mitaala ya shule ikajumuisha dhana hii kama mambo mtambuka katika jamii.

Mwisho, tujifunze kumrudia MUNGU kwa namna zozote ziwazo kama ni kwa kupitia dini asili au dini za kisasa lakini lengo likibaki kuwasaidia na kuwaokoa ndugu zetu.

Chagizo: kama Ualbino unaleta utajiri kweli, ni nini nafasi ya Wazungu na wale maalbino waliopo sehemu nyingine?