Australia na Pasifiki : Tofauti kati ya masahihisho
TjBot (majadiliano | michango) d r2.7.2) (Roboti: Imeongeza gn:Oseania |
d r2.7.2) (Roboti: Imebadilisha: mn:Австрали ба далайн орнууд |
||
Mstari 367: | Mstari 367: | ||
[[mk:Океанија]] |
[[mk:Океанија]] |
||
[[ml:ഓഷ്യാനിയ]] |
[[ml:ഓഷ്യാനിയ]] |
||
[[mn:Австрали ба |
[[mn:Австрали ба далайн орнууд]] |
||
[[mr:ओशनिया]] |
[[mr:ओशनिया]] |
||
[[ms:Oceania]] |
[[ms:Oceania]] |
Pitio la 09:35, 27 Agosti 2012
Australia na Visiwa vya Pasifiki (pia: Oceania, Okeania, Oshania) hujumlishwa mara nyingi pamoja katika hesabu ya mabara. Hasa watu kwenye visiwa vingi vya Pasifiki vina utamaduni wa karibu. Historia ya visiwa hivi kabla ya kuenea kwa ukoloni imefanana katika mengi.
Bara au la
Hivyo mara nyingi sehemu hii ya dunia ime itwa "Bara la Kiutamaduni". Jina hili si sahihi kijiografia kwa sababu maeneo yake yapo juu ya mabamba ya gandunia tofauti kama vile bamba la Pasifiki, bamba la Australia na mengine madogo. Hata wataalamu hawapatani kuhusu mipaka ya eneo hili.
Jina
Kwa lugha nyingi za dunia jina la "Oceania" (Okeania, Oshania) limekuwa kawaida kutokana na neno la Kigiriki "okeanos" (kilatini: oceanus, Kiingereza ocean). Hivyo "Oceania" yamaanisha "nchi katika bahari". Ila tu hatuoni faida ya kuingiza neno hili katika lugha ya Kiswahili kwa sababu ni neno lisiloeleweka vizuri. Mara wataalamu hujadili "Oceania" kuwa visiwa vya Pasifiki pamoja na Australia; mara wanaona "Oceania" ni visiwa vile pekee bila Australia na wengine wanasema wenyewe "visiwa vya Pasifiki" ingekuwa jina nzuri zaidi kama Australia haihesabiwi.
"Australasia" imekuwa jaribio tofauti ya kutaja eneo hasa kati ya wataalamu wa Australia ila tu haipendwi na watu wengi visiwani. Hivyo imetumiwa zaidi kwa kanda la Australia na visiwa jirani pekee.
Eneo
Visiwa vyote kwa pamoja (bila Australia yenyewe) hukadiriwa kuwa 7,500 vyenye eneo la nchi kavu la kilomita za mraba milioni 1.3 vilivyosambaa katika eneo la bahari la kilomita za mraba milioni 70. Takriban visiwa 2,100 vimekaliwa na watu milioni 14.9.
Kanda
Mara nyingi kanda nne zimetofautishwa:
Maneneo yanayotajwa kwa "Melanesia" na "Australasia" huingiliana.
Nchi na Maeneo ya Australia na Visiwa vya Pasifiki
(Nchi huru zaonekana kwa mwandiko mzito, maeneo yaliyo chini ya nchi nyingine kwa mwandiko wa kawaida)
Jina la eneo, pamoja na bendera[1] |
Eneo (km²) |
Wakazi (kadiro mnamo 1 Julai 2002) |
Msongamano (watu kwenye km²) |
Mji mkuu |
---|---|---|---|---|
Australasia (Australia na New Zealand) | ||||
Australia | 7,686,850 | 20,697,241 | 2.5 | Canberra |
Kisiwa cha Krismasi (Australia)[2] | 135 | 474 | 3.5 | The Settlement |
Visiwa vya Cocos (Keeling) (Australia)[2] | 14 | 632 | 45.1 | West Island |
New Zealand[3] | 268,680 | 3,908,037 | 14.5 | Wellington |
Kisiwa cha Norfolk (Australia) | 35 | 1,866 | 53.3 | Kingston |
Melanesia[4] | ||||
Fiji | 18,270 | 856,346 | 46.9 | Suva |
Sehemu za Indonesia[5] | 499,852 | 4,211,532 | 8.4 | Jakarta |
Kaledonia Mpya (Ufaransa) | 19,060 | 207,858 | 10.9 | Nouméa |
Papua Guinea Mpya[6] | 462,840 | 5,172,033 | 11.2 | Port Moresby |
Visiwa vya Solomon | 28,450 | 494,786 | 17.4 | Honiara |
Vanuatu | 12,200 | 196,178 | 16.1 | Port Vila |
Mikronesia | ||||
Shirikisho la Mikronesia | 702 | 135,869 | 193.5 | Palikir |
Kiribati | 811 | 96,335 | 118.8 | Teinainano |
Visiwa vya Marshall | 181 | 73,630 | 406.8 | Majuro |
Nauru | 21 | 12,329 | 587.1 | Yaren |
Visiwa vya Mariana ya Kaskazini Marekani | 477 | 77,311 | 162.1 | Saipan |
Guam (Marekani) | 549 | 160,796 | 292.9 | Hagåtña |
Palau | 458 | 19,409 | 42.4 | Melekeok[7] |
Polynesia[8] | ||||
Samoa ya Marekani (Marekani) | 199 | 68,688 | 345.2 | Fagatogo, Utulei[9] |
Visiwa vya Cook (New Zealand) | 240 | 20,811 | 86.7 | Avarua |
Polynesia ya Kifaransa (Ufaransa) | 4,167 | 257,847 | 61.9 | Papeete |
Hawaii (Marekani) | 29,311 | 1,211,537 | 42.75 | Honolulu |
Niue (New Zealand) | 260 | 2,134 | 8.2 | Alofi |
Kisiwa cha Pasaka (Chile) | 163,6 | 3,791 | 23,17 | Hanga Roa |
Visiwa vya Pitcairn (Uingereza) | 5 | 47 | 10 | Adamstown |
Samoa | 2,944 | 178,631 | 60.7 | Apia |
Tokelau (New Zealand) | 10 | 1,431 | 143.1 | —[10] |
Tonga | 748 | 106,137 | 141.9 | Nuku'alofa |
Tuvalu | 26 | 11,146 | 428.7 | Vaiaku |
Wallis na Futuna (Ufaransa) | 274 | 15,585 | 56.9 | Mata-Utu |
Total | 9,008,458 | 35,834,670 | 4.0 |
Notes:
- ↑ Maeneo hutajwa kufuatana na mpangilio wa Umoja wa Mataifa. Maeneo kadhaa huhesabiwa ama kama nchi za kimabara au sehemu za Asia au Amerika Kaskazini.
- ↑ 2.0 2.1 Kisiwa cha Krismasi na Visiwa vya Cocos (Keeling) ni maeneo ya Australia katika Bahari Hindi kusini ya Indonesia hivyo hutazamia kuwa sehemu za Asia ya Kusini-Magharibi.
- ↑ New Zealand mara nyingi huhesabiwa ndani ya Polynesia kuliko Australasia.
- ↑ Bila Timor ya Mashariki na sehemu za Indonesia ambazo ni visiwa vya Asia lakini huhesabiwa mara nyingi kati ya visiwa vya Pasifiki.
- ↑ <-- Indonesia kwa jumla ni sehemu ya Asia ya Kusini-Mashariki; sehemu za Guinea Mpya (Irian Jaya) na Visiwa vya Maluku .huhesabiwa humo
- ↑ [[Papua Guinea Mpya huhesabiwa upande wa Australia lakini pia kwa Melanesia.
- ↑ Tar 7 Oktoba 2006 serikali ilihamia Melekeok iliyoko takriban kilomita 20 kaskazini ya Koror.
- ↑ Bila Hawaii ambalo ni jimbo la Marekani. Inahesabiwa mara nyingi kati ya eneo la Amerika ya Kaskazini ingawa ni funguvisiwa ndani ya Pasifiki.
- ↑ Fagatogo ni makao ya unge na mahakama ya Samoa ya Marekani; Utulei ni makao ya serikali.
- ↑ Tokelau ni eneo la New Zealand na haina makao makuu kwa jumla kila kisiwa kina chake.