T-Pain : Tofauti kati ya masahihisho
d r2.7.1) (roboti Nyongeza: simple:T-Pain |
d r2.7.2) (Roboti: Imeongeza ca:T-Pain |
||
Mstari 48: | Mstari 48: | ||
[[ar:تي-بين]] |
[[ar:تي-بين]] |
||
[[ca:T-Pain]] |
|||
[[cs:T-Pain]] |
[[cs:T-Pain]] |
||
[[da:T-Pain]] |
[[da:T-Pain]] |
Pitio la 09:06, 8 Julai 2012
T-Pain | |
---|---|
| |
Maelezo ya awali | |
Jina la kuzaliwa | Faheem Rasheed Najm |
Amezaliwa | 30 Septemba 1985 Tallahassee, Florida, U.S. |
Aina ya muziki | R&B, hip hop |
Kazi yake | Mwimbaji-mtunzi, rapa, mtayarishaji wa rekodi, dansa |
Ala | Kinanda |
Miaka ya kazi | 2004–mpaka sasa |
Studio | Nappy Boy, Konvict, Jive |
Ame/Wameshirikiana na | Akon, Chris Brown, Tay Dizm, Young Jeezy, DJ Khaled, Flo Rida, Lil Wayne, Ludacris, Plies, Rick Ross, Kanye West, Twista, Travis McCoy, Lil Mama, The Lonely Island |
Tovuti | www.t-pain.net |
Faheem Rasheed Najm (amezaliwa tar. 30 Septemba, 1985) ni mwimbaji-mtunzi, rapa, na mtayarishaji wa rekodi kutoka nchini Marekani. Anafahamika zaidi kwa jina la kisanii kama T-Pain. Ameanza shughuli za urapa akiwa katika kundi la Nappy Headz. Mnamo mwaka wa 2005, akawa mwimbaji na kuweza kutoa albamu yake ya kwanza iliyoitwa Rappa Ternt Sanga ikiwa na vibao vyake vikali vya "I'm Sprung" na "I'm N Luv (Wit A Stripper)". Shughuli zake kama mwimbaji, T-Pain ametumia sana kionjo cha sauti cha Auto-Tune. Tangu kutolewa kwa albamu yake ya kwanza, T-Pain ametayarisha vibao kadhaa vikali vyake mwenyewe na vya marapa na waimbaji wengine wa R&B. T-Pain pia amekuwa na single kumi kwenye chati za Billboard Hot 100. Mnamo mwaka wa 2008, ameshinda tuzo ya Grammy na rapa Kanye West kwa ajili ya single ya "Good Life". Mnamo mwaka wa 2010 ameshinda tuzo nyingine ya Grammy na Jamie Foxx kwa ajili ya single ya "Blame It". T-Pain pia ni mwanzilishi wa studio ya kurekodia ya Nappy Boy Entertainment, imeanzishwa mwaka wa 2005.
Wasifu
Maisha ya awali
Najm alizaliwa mjini Tallahassee, Florida.[1] Jina lake la kisanii ni kifupi cha "Tallahassee Pain" ("Tallahassee Mauimivu) na amechagua jina hilo kwa sababu ya ugumu wa maisha aliyoyapata wakati anaishi huko.[2]
Kazi
Diskografia
- Rappa Ternt Sanga (2005)
- Epiphany (2007)
- Thr33 Ringz (2008)
- RevolveR (2010)
Marejeo
- ↑ T-Pain Gets Some Heat For Turning Gospel Song Into 'Alcoholic Anthem'.. Retrieved August 28, 2008.
- ↑ Koha, Nui Te. "Escaping Tallahassee", Herald Sun, 2007-06-10. Retrieved on 2008-12-10.