Kicheche : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
dNo edit summary |
Nyongeza jamii |
||
Mstari 39: | Mstari 39: | ||
[[Jamii:Mbwa na jamaa]] |
[[Jamii:Mbwa na jamaa]] |
||
[[Jamii:Wanyama wa Afrika]] |
Pitio la 22:37, 31 Januari 2012
Kicheche | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kicheche-nyoka (Poecilogale albinucha)
| ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Vicheche au cheche ni wanyama wa jenasi mbalimbali katika familia Mustelidae. Wanyama hawa ni miongoni mwa wale wanaotoa vundo mbaya kabisa. Wataalamu wengine wanadai kwamba kicheche wa kawaida ananuka vibaya kuliko wanyama wote. Vundo hii inatoka matezi karibu na mkundu kama mnyama akitishwa, na kwa kawaida adui atoroka. Spishi zote zina pua, kidari, tumbo na miguu nyeusi. Zile za Afrika zina milia myeupe na myeusi mgongoni, zile za Amerika zina mgongo kijivu na ile ya Ulaya ina mgongo njano wenye madoa meusi. Vicheche hula wanyama, ndege na mijusi wadogo, wadudu, samaki, amfibia, nyoka na hata matunda na manyasi.
Spishi za Afrika
- Ictonyx libycus, Kicheche-jangwa (Sahara Striped Polecat)
- Ictonyx striatus, Kicheche wa Kawaida (Striped Polecat or Zorilla)
- Poecilogale albinucha, Kicheche-nyoka (African Striped Weasel)
Spishi za mabara mengine
- Galictis cuja, Kicheche Mdogo wa Amerika (Lesser Grison)
- Galictis vittata, Kicheche Mkubwa wa Amerika (Greater Grison)
- Vormela peregusna, Kicheche Madoa (Marbled Polecat)
Picha
-
Kicheche mdogo wa Amerika
-
Kicheche mkubwa wa Amerika
-
Kicheche madoa