Mfumo wa Jua : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
No edit summary
d r2.6.4) (roboti Nyongeza: kk:Күн жүйесі
Mstari 193: Mstari 193:
[[jv:Tata Surya]]
[[jv:Tata Surya]]
[[ka:მზის სისტემა]]
[[ka:მზის სისტემა]]
[[kk:Күн жүйесі]]
[[km:ប្រព័ន្ធព្រះអាទិត្យ]]
[[km:ប្រព័ន្ធព្រះអាទិត្យ]]
[[kn:ಜ್ಯೋತಿರ್ಮಂಡಲ]]
[[kn:ಜ್ಯೋತಿರ್ಮಂಡಲ]]

Pitio la 20:08, 20 Agosti 2011

Jua letu na sayari zake

Mfumo wa jua na sayari zake ni utaratibu wa jua letu na sayari au sayari kibete zinazolizunguka pamoja na miezi yao, asteroidi, meteoridi, kometi na vumbi ya angani yote ikishikwa na mvutano wa jua.

Kwa kawaida huhesabiwa sayari 9 zinazozunguka jua. Lakini miaka ya nyuma magimba makubwa yamegunduliwa angani ambayo bado hayakukubaliwa kama yahesabiwe kuwa sayari au aina ya asteoridi.

Orodha inayofuata bado inahitaji kuangaliwa kwa sababu kuna tofauti kati ya kamusi na vitabu mbalimbali jinsi ya kutaja sayari fulani.

Sayari za jua letu

Sayari katika mfumo wa jua ni zifuatazo:

Namba zote zinazotaja sifa mbalimbali za sayari zinaonyesha kipimo kulingana na tabia za dunia yetu kuwa "1". Kuhusu majina ya sayari kadhaa kuna mchanganyiko katika kamusi na vitabu. Pale ambako jina au umbo tofauti la jina ni kawaida linaonyeshwa katika mabano kama (jina). Majina yanayotumiwa katika vitabu kadhaa bila kuwa na uhakika yanaonyeshwa katika mabano ya italiki pamoja na alama ya swali kama (? jina). [1]

* Utaridi ni jina la sayari ya kwanza kutokana na lugha ya Kiarabu. Vitabu vingine hutumia neno "Zebaki" ni pia neno lenye asili ya Kiarabu linalomaanisha metali; inaonekana limepatikana kama tafsiri ya jina la Kiingereza la sayari ya kwanza "Mercury" bila kujua historia ya majina ya sayari sita ya kwanza yaliyoingia katika Kiswahili kutoka lugha ya Kiarabu. [2]
** Zuhura - Ng'andu ni sayari lenye jina la Kibantu kwa Kiswahili pamoja na jina la asili ya Kiarabu
*** Tazama makala ya Dunia kwa ajili ya namba halisi. Neno "ardhi" hutumika na waandishi kadhaa badala ya "dunia" wakitaka kutaja sayari ya tatu.
**** Tangu 2006 Pluto imeingizwa katika kundi la "sayari kibete".
Jina la sayari Kipenyo kwenye ikweta
kulingana na kipenyo cha dunia = 1
Masi Nusukipenyo ya mzingo wa kuzunguka jua Muda wa mzingo
(miaka)
Kuinama kwa mzingo wa kuzunguka jua
Pembenukta (°)
Muda wa siku ya sayari
(siku)
Miezi
Utaridi (Zebaki)* 0.382 0.06 0.387 0.241  7.00 58.6 0
Zuhura (Ng'andu)** 0.949 0.82 0.72 0.615  3.39 -243 0
Dunia (Ardhi)*** 1.00 1.00 1.00 1.00  0.00 1.00 1
Meriki 0.53 0.11 1.52 1.88  1.85 1.03 2
Mshtarii (? Sumbula) 11.2 318 5.20 11.86  1.31 0.414 63
Zohari (Zohali) (? Sarateni) 9.41 95 9.54 29.46  2.48 0.426 49
Uranus (? Zohali) 3.98 14.6 19.22 84.01  0.77 -0.718 27
Neptun (? Kausi) 3.81 17.2 30.06 164.8  1.77 0.671 13
Pluto (? Utaridi)**** 0.18 0.002 39.5 248.5 17.1     -6.5 3

Marejeo

  1. Linganisha ukuasa wa majadiliano:sayari
  2. kuhusu majina ya sayari zilizojulikana kwa Waswahili na hivyo kuwa na majina ya asilia linganisha Jan Knappert, Swahili Islamic poetry, Brill 1971, Vol 1 uk 96-97 - taz google booksearch [1]
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mfumo wa Jua kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA