Hungaria : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.6.2) (roboti Nyongeza: xmf:უნგრეთ
Mstari 94: Mstari 94:
[[Jamii:Hungaria|*]]
[[Jamii:Hungaria|*]]
[[Jamii:Nchi za Ulaya|H]]
[[Jamii:Nchi za Ulaya|H]]

[[xmf:უნგრეთ]]


[[ab:Мадиартәыла]]
[[ab:Мадиартәыла]]
Mstari 185: Mstari 187:
[[kk:Мажарстан]]
[[kk:Мажарстан]]
[[kl:Ungarni]]
[[kl:Ungarni]]
[[km:ប្រទេសហុងគ្រី]]
[[ko:헝가리]]
[[ko:헝가리]]
[[koi:Мадьярму]]
[[koi:Мадьярму]]
Mstari 287: Mstari 290:
[[wuu:匈牙利]]
[[wuu:匈牙利]]
[[xal:Хунһармудин Орн]]
[[xal:Хунһармудин Орн]]
[[xmf:უნგრეთ]]
[[yi:אונגארן]]
[[yi:אונגארן]]
[[yo:Húngárì]]
[[yo:Húngárì]]

Pitio la 12:57, 18 Julai 2011

Hungaria

Hungaria (Magyarország) ni nchi ya Ulaya ya Kati. Mji mkuu ni Budapest. Nchi ina wakazi milioni 10. Imepakana na Austria, Slovakia, Ukraine, Romania, Serbia, Kroatia na Slovenia.

Miji muhimu baada ya Budapest ni Miskolc, Debrecen, Szeged, Pécs, Győr na Szolnok.

Kihungaria ni lugha rasmi.

Historia

Hungaria ilitokea kama nchi ya pekee wakati wa karne ya 10 BK. Tangu zamani za kuzaliwa kwake Kristo (milenia ya kwanza) sehemu kubwa ya Hungaria ilijulikana kama Panonia ikawa sehemu ya Dola la Roma. Tangu kuporomoka kwa nguvu ya Waroma ilivamiwa na makabila mbalimbali kama vile Wagermanik, Wahunni na Waslavi.

Baada ya mwaka 900 Wahungaria chini ya mtemi Arpad walivamia eneo hili. Wakati ule Wahungaria walikuwa mkusanyo wa makabila wahamiaji waliojiita "Majari" (Magyar) waliotoka katika maeneo kati ya mto Volga na milima ya Ural. Kutoka makazi yao mapya katika Panonia waliendelea kuvamia maeneo mengine ya Ulaya hadi milima ya Pirenei. Baada ya kushindwa na Wajerumani mwaka 955 walibaki katika makazi yao na mnamo mwaka 1000 mfalme Stefano (Ishtvan) alipokea ubatizo akaongoza taifa lake kuingia katika Ukristo.

Wakati wa uvamizi wa Wamongolia baada ya Chingis Khan katika karne ya 13 nchi iliangamizwa na nusu ya wakazi wakauawa. Baadaye wafalme Wahungaria waliwakaribisha walowezi kutoka Ujerumani walioanzisha vijiji vingi na pia miji.

Wakati wa karne ya 15 Waosmani walianza kuenea kwenye Balkani wakaingia katika Hungaria kutoka upande wa mashariki. Katika mapigano ya Mohacs mwaka 1526 Hungaria ilishindwa na sehemu kubwa ikawa chini ya Waosmani. Magharibi ya nchi ikaendelea kuitwa ufalme wa Hungaria lakini ufalme uliingia mkononi mwa nyumba ya Habsburg yaani chini ya watawala wa Austria.

Katika karne zilizofuata watawala wa Habsburg walirudisha Waosmani nyuma na ufalme wa Hungaria ikawa sehemu ya milki ya Habsburg yaani Austria. Katika karne ya 19 mnamo 1848 Wahungaria waliasi dhidi ya watawala lakini walishindwa. Lakini Kaisari Franz Joseph I alibadilisha siasa akatafuta usaidizi wa Wahungaria katika utawala wa ufalme. Katiba mpya iliunda cheo cha sawa kati ya Austria na Hungaria chini ya mtawala yeye yule mwenye vyeo vya Kaisari wa Austria na Mfalme wa Hungaria na milki ikaitwa "Austria-Hungaria".

Austria-Hungaria ilikuwa milki kubwa katika Ulaya ya Kati na Mashariki kati ya 1867 hadi 1918. Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia milki ikaporomoka na Hungaria ikaendelea kama nchi ya pekee yenye katiba ya ufalme lakini bila mfalme. Katika vita kuu ya pili ya dunia Hungaria ikaingia kwa upande wa Ujerumani ukaendelea kuwatesa Wayahudi wake wa kushikamana na siasa ya Hitler na mwishowe ikashindwa pamoja na Ujerumani. Hungaria ikavamiwa na jeshi la Umoja wa Kisovyeti na mabwana hao wapya walihakikisha ya kwamba chama cha kikomunisti ilishika serikali. Hungaria ikawa sehemu ya Mapatano ya Warshawa ikasimama upande wa mashaki katika kipindi cha vita baridi. Mwaka 1956 wananchi wengi walipindua serikali ya kikomunisti na serikali mpya chini ya Imre Nagy ilianzisha demokrasia ya vyama vingi. Lakini wanajeshi wa Kisovyti wakaingia kati wakarudisha utawala wa chama cha kikomunisti ulioendelea hadi kuporomoka kwa ukomunisti mnamo 1989.

Hungaria imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 2004.

Jiografia

Tazama pia

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hungaria kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.