Mtume Barnaba : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.7.1) (roboti Nyongeza: mk:Апостол Варнава
d r2.7.1) (roboti Nyongeza: id:Barnabas
Mstari 39: Mstari 39:
[[fi:Barnabas]]
[[fi:Barnabas]]
[[fr:Barnabé]]
[[fr:Barnabé]]
[[id:Barnabas]]
[[it:Barnaba apostolo]]
[[it:Barnaba apostolo]]
[[ja:バルナバ]]
[[ja:バルナバ]]

Pitio la 09:12, 24 Aprili 2011

Kifodini cha Mt. Barnaba, kutoka Legenda Aurea ya Jacopo wa Varazze.

Yosefu wa Kupro, Myahudi wa kabila la Lawi, anajulikana hasa kupitia kitabu cha Matendo ya Mitume.

Humo tunapata habari kuwa aliongokea mapema Ukristo, akauza shamba lake na kuwakabidhi Mitume wa Yesu mapato yake ili wawasaidie maskini. Labda kwa sababu hiyo Mitume walimuita Barnaba, yaani "Mwana wa faraja" (Mdo 4:36-37).

Kisha kuheshimiwa hivyo katika Kanisa la awali huko Yerusalemu, alimtambulisha na kumdhamini Mtume Paulo muda mfupi baada ya huyo kuongoka huko Damasko (Mdo 9:26-28).

Watu wa mataifa walipoanza kuingizwa moja kwa moja katika Ukristo huko Antiokia, alitumwa huko kwa niaba ya Kanisa mama, akawa kiongozi mkuu wa jumuia hiyo mpya (Mdo 11:19-30; 13:1).

Baadaye Roho Mtakatifu alidai yeye na Paulo wapelekwe kufanya umisionari sehemu nyingine, wakaondoka pamoja na binamu yake, Yohane Marko, kuelekea kwanza kisiwani Kupro, halafu bara, katika maeneo ya Uturuki Kusini wa leo (Mdo 13:2-14:28).

Kazi yao ilipopata upinzani kwa kutodai Wapagani wakiongoka washike Torati yote, walikwenda pamoja Yerusalemu (mwaka 49 hivi, kwa mtaguso wa Mitume, ambao uliamua kuhusu suala hilo (Mdo 15:1-35).

Baada ya kutengana na Paulo, Barnaba alifunga tena safari kwenda Kupro pamoja na Marko (Mdo 15:36-39) kati ya miaka 50 na 53, na baada ya hapo hatuna tena habari ya hakika juu yake.

Kanisa Katoliki na Waorthodoksi wanamheshimu kama mtakatifu tarehe 11 Juni.

Wataalamu wengine wanamtaja kama mtunzi wa Waraka kwa Waebrania, na Klemens wa Aleksandria alimtaja kama mwandishi wa Waraka wa Barnaba, lakini hakuna hakika.